• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma aagiza watendaji kusimamia utunzaji vyanzo vya maji

Imewekwa kuanzia tarehe: January 31st, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewaagiza maafisa Tarafa na viongozi wote ngazi ya Wilaya kusimamia utunzaji wa vyanzo vya maji ili viwe endelevu.

Mndeme ametoa agizo hilo wakati anafungua mkutano wa wadau wa sekta ya maji mkoani Ruvuma kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mndeme pia ameagiza wote wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye vyanzo vya maji kuondolewa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004 ya sheria ya RUWASA ya mwaka 2019.

Maagizo mengine yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa katika kikao hicho ni Halmashauri zote na sekretarieti ya Mkoa kuwajibika kikamilifu katika kutekeleza na kusimamia majukumu yote yaliyoorodheshwa kwenye sheria namba tano ya huduma ya maji ya mwaka 2019.

“Mameneja wa RUWASA Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri zote zihakikishe kwamba miradi iliyopo na mingine itakayojengwa inaunda vyombo huru vya watumiaji maji kwa sheria namba tano ya mwaka 2019 kabla au ifikapo Mei 31,2021’’,alisisitiza Mndeme.

Mndeme pia ameagiza katika kikao cha Baraza la madiwani cha kila robo katika Halmashauri zote iwepo mada ya kudumu ambapo Mameneja wa RUWASA katika wilaya husika watatoa taarifa kuhusu hali ya upatikanaji na usajili wa vyombo vya watumiaji maji.

Mkuu wa Mkoa pia ameagiza  RUWASA Wilaya na Mkoa  zishirikiane na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa mazingira SOUWASA sanjari na ofisi za mabonde ya maji katika kutafuta vyanzo vya maji na kuandaa mipango ya utunzaji wa vyanzo vya maji.

“Naagiza fedha zitokanazo na mauzo ya maji zikaguliwe na mkaguzi wa ndani wa Halmashauri ili kujiridhisha namna fedha hizo zilivyotumika,endeleeni kuwachukulia hatua wanaoharibu kwa makusudi miundombinu ya maji na vyanzo vya maji’’,alisema Mndeme.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira vijijini (RUWASA) Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshonga ameyataja majukumu ya RUWASA kuwa ni kuandaa mipango ya kusanifu miradi,kujenga na kusimamia uendeshaji wake.

Majukumu mengine ni kuendeleza vyanzo vya maji kwa kufanya utafiti wa maji chini ya ardhi,kuchimba visima na kujenga mabwawa sanjari na kufanya matengenezo makubwa ya miundombinu ya maji.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Januari 30,2021 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.