• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma ahimiza kasi ya ujenzi madarasa ya UVIKO Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: November 30th, 2021

MKUU wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,amewaagiza viongozi wa wilaya ya Namtumbo kuongeza kasi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na miundombinu mingine ya elimu kukamilika kabla ya Tarehe 10 Mwezi Desemba mwaka huu.

Ibuge ametoa agizo hilo jana, wakati akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa vinavyojengwa kupitia mpango wa maendeleo wa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya Covid 19 wilayani humo.

Mkuu wa mkoa alisema,hajaridhishwa na  na kasi ya utekelezaji wa miradi ya Covid -19 katika wilaya hiyo kwa kuwa,bado ujenzi wake  unakwenda kwa kusua sua  ikilinganisha na miradi inayojengwa kwenye  wilaya nyingine, ambapo ametoa wiki mbili  wawe wamekamilisha kazi hiyo.

“ maeneo mengine nimekuta mafundi zaidi ya mmoja katika  darasa ,kuna wanaopiga lipu,kufunga milango,madirisha, na kupaua lakini katika miradi yenu hapa mafundi ni wachache,kwa hiyo naagiza miradi yote iwe imekamilike kabla ya tarehe 10 Desemba” alisema Ibuge.

Aidha amewataka viongozi wa wilaya hiyo, kuhakikisha vifaa vinavyotumika katika ujenzi huo vinakuwa na ubora unaotakiwa ili kuwezesha kupata madarasa bora na viwango vya hali ya juu badala ya kujenga kwa kubabaisha.

Ibuge,ametaka kila mmoja kusimamia miradi hiyo kwenye eneo lake ili wanafunzi wote watakaochaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari mwezi Januari mwakani wapate nafasi kwenye shule watakazopangiwa.

Jenerali Ibuge alisema,Serikali imetoa fedha nyingi za miradi  kwa Halmashauri hiyo zikiwemo za utekelezaji wa miradi ya Covid-19 na  lengo ni kuhakikisha miundombinu ya elimu ina kuwa bora na wanafunzi wanapata fursa ya kusoma na kufanya vizuri kwenye masomo.

Katika ziara hiyo ambayo alifuatana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, alitembelea shule ya sekondari Nanungu,Mtakanini,Msindo, Nasuli na Narwi ambazo ujenzi wake uko katika hatua mbalimbali.

Mbunge wa Jimbo la Namtumbo Vita Kawawa, ameishukuru serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye sekta ya elimu na afya ambayo itaongeza morali ya wanafunzi kusoma kwa bidii.

Hata hivyo alisema, changamoto kubwa ni kuchelewa kwa ujenzi wa miradi hiyo kutokana na upatikanaji wa vifaa kutoka kwa wafanya biashara waliopandisha bei ya vifaa.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya hiyo Dkt Julius Ningu alisema,watafanyia kazi maelekezo ya Mkuu wa mkoa na kuhaidi ujenzi wa vyumba vya madarasa vinavyojengwa  vitakamilika kwa muda uliopangwa.

Mkuu wa shule ya sekondari Mtakanini Michael Kabogo alisema, wamepokea jumla ya Sh.milioni 40 kwa ajili ya kujenga vyumba viwili vya madarasa na hadi sasa fedha zilizotumika ni Sh. 12,937,700 na salio Sh.27,062,300.

MWISHO.




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.