• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma akabidhi msaada wa taulo za kike 2,502 kwa wanafunzi Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: December 11th, 2020


MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amekabidhi msaada wa taulo za kike 2,502 zilizotolewa na Shirika la Social Action Trust Fund(SATF) kwa wanafunzi wa shule saba za msingi wilayani Nyasa.

Mndeme amemkabidhi taulo hizo na nguo za ndani 834 Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isebala Chilumba katika hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea.

Mndeme amezitaja shule ambazo zitakabidhiwa msaada huo kuwa ni  zenye wanafunzi wa darasa la nne hadi la sita  kutoka shule saba za msingi ambazo ni shule ya msingi, Kilosa, Likwilu, Muongozo,Ukuli,Kuhamba,Liparamba na Lumeme.

“Natoa wito kwa Halmashauri ya Nyasa,kuhakikisha inashirikiana na Shirika la SATF,kabla ya matumizi ya vifaa wanafunzi wapewe mafunzo kupitia klabu zao za afya’’,alisisitiza Mndeme.

Amesema  kutolewa kwa vifaa hivyo ni  juhudi za serikali za kuhakikisha kunakuwa na mazingira wezeshi ya kumhakikishia mtoto wa kike anapata elimu kwa kuhudhuria masomo na anadumu shuleni na kuhitimu masomo yake bila vikwazo.

Naye Afisa Miradi wa SATF Makao makuu Edgar Kihwelo amesema shirika hilo linafanya kazi na  Asasi za kiraia 19 katika mikoa 16 na wilaya 32 za Tanzania Bara.

Amesema tangu kuanzishwa kwa Shirika hilo  watoto wanaishi katika mazingira magumu 193,000 wamesaidiwa na kuwawezesha kupata elimu na kaya zipatazo 900 zimejengewa uwezo kiuchumi.

Kulingana na Kihwelo,katika wilaya ya Nyasa kwenye mradi ulianzishwa mwaka 2019,Shirika limeweza kusaidia watoto wa shule za msingi 103 na watoto wa shule za sekondari  sekondari 80.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo ,Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba amelishukuru Shirika la SATF kwa msaada huo ambao amesema utasaidia kumkomboa mtoto wa kike kielimu na kufikia ndoto zao.

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Ruvuma Imanuel Kisongo amelipongeza Shirika la SATF kwa kuunga mkono jitihada za serikali za kumkomboa mtoto  wa kike katika Mkoa wa Ruvuma.

Amesema taulo za kike zitamhakikisha mtoto wa kike anahudhuria masomo hata  katika siku zake za hedhi bila kuathiri masomo yao na kutimiza malengo yao kimaisha.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Desemba 11,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.