• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma awaapisha wakuu wapya wa wilaya

Imewekwa kuanzia tarehe: June 22nd, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amewaapisha Wakuu wa Wilaya wapya,  nakutoa maelekezo katika utendaji kazi wao.

Hafla  ya kuwaapisha Wakuu wa Wilaya imefanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu  wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali.

RC Ibuge amewaagiza Wakuu wa Wilaya wahakikishe wanasimamia wananchi kushiriki katika masuala ya Ulinzi na Usalama katika maeneo yao,  kwa sababu hakuna maendeleo bila kuwa Ulinzi na Usalama.

“kasimamieni maendeleo ya kiuchumi na kijamii, hakikisheni  Miradi yote inayotekelezwa katika maeneo yenu, inakuwa yenye tija na kukamilika kwa wakati”. alisisitiza RC Ibuge.

 Maagizo mengine aliyoyatoa Mkuu wa Mkoa kwa Wakuu wa Wilaya ni kuhakikisha thamani ya fedha katika Miradi inaonekana, kuhakikisha uwepo wa   matumizi sahihi ya miradi iliwekezwa na Serikali na kuondoa na vikwazo katika ufanyaji biashara na kuhakikisha huduma zinapatikana kwa wakati na haraka.

RC Ibuge pia amewaagiza Wakuu wa Wilaya  kusimamia uwezeshaji wa Makundi maalum, ambayo ni wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, kwa kuhakikisha asilimia 10 ya fedha ya mapato ya ndani, inatengwa kwa ajili ya kundi hilo.

Mkuu wa Mkoa amewataka Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao wakahamasishe wananchi kujiunga na Bima ya Afya iliyoboreshwa, na kuhakikisha Fedha inayotakiwa kununuliwa madawa inawekwa benki.

Amesisitiza kuhakikisha Mazao ya kimkakati  Soya, Ufuta, Mbaazi, Choroko na Korosho Kuuzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani, ili wakulima watimize ndoto zao, Pamoja  na kusimamia utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Taasisi za Umma zilizopo katika Halmashauri.

Ibuge amewaagiza Wakuu wa Wilaya  kutatua kero za wananchi, na kusimamia ukusanyaji wa mapato na matumizi sahihi ya fedha za umma, kusimamia masuala ya elimu, na matumizi bora ya pembejeo za kilimo na elimu ya biashara na ujasiliamali kwa ajili ya kuboresha kipato kwa wananchi.

Kwa upande wake  Mkuu Mpya wa Wilaya  ya Nyasa Kanali  Laban Thomas akizungumza baada ya kuapishwa, amehaidi kuwa Mtumishi, na kutokuwa mtawala  na kujifunza kutoka kwa wananchi pamoja na kuchukua changamoto zao na kuzifanya kuwa fursa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Julius Ningu ameahidi kushughulikia changamoto zinazowakabili wanachi wa Namtumbo na anatarajia kujifunza mengi kutoka kwa wananchi wenyewe.

Mkoa wa Ruvuma una wilaya tano ambazo ni Songea, Tunduru, Namtumbo,Mbinga na Nyasa.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Juni 22,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.