• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma awataka watumishi kwenda kwa wananchi

Imewekwa kuanzia tarehe: August 26th, 2022

MKUU wa mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas,amewataka viongozi wa umma  kwenda vijiji ili kutambua,kutatua shida na kuwaletea  wananchi maendeleo,badala ya kutumia muda mwingi kukaa ofisini.Kanali Laban ametoa kauli hiyo  kwa nyakati tofauti,wakati akizungumza na wananchi na viongozi wa wilaya ya Mbinga na Nyasa  akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha wananchi kujiandaa na kushiriki kikamilifu zoezi la sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika tarehe  23(kesho).

“watendaji wa umma acheni mambo ya kizamani ya kuvaa tai muda wote mkiwa ofisini,nendeni vijijini ili kuwasilikiza, kutatua kero na kuwaletea  maendeleo wananchi mnaowaongoza”alisema.

Alisema, watumishi na viongozi wana wajibu wa kuitumikia jamii  hasa katika maeneo ya vijijini ambako bado kuna changamoto nyingi na sio kukaa ofisini huku wamevaa tai na suti.

Aliongeza kuwa,viongozi wa aina hiyo hawana nafasi katika mkoa huo hivyo  kwa kuwa hawatendi haki kwa wananchi na Rais Samia SuluhuHassan anayepambana usiku na mchana kutatua kero  na kuboresha hali ya maisha kwa watu wake.

Laban alisema,wananchi wanahitaji sana kupata msaada na mchango wa viongozi wao kwa ajili ya kutatua kero na changamoto zinazowakabili katika maeneo yao na siyo kutanguliza maslahi binafsi.

Amewataka kushirikiana na wananchi katika maeneo yao,kubuni na kutafuta vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitachochea kukua kwa uchumi na kuboresha huduma mbalimbali za kijamii.

Akiwa katika wilaya ya Nyasa,Mkuu wa mkoa amewakumbusha wananchi wa wilaya hiyo kuhakikisha wanatunza chakula walichovuna katika msimu wa kilimo 2021/2022 kama tahadhari  ya kukabiliana na uhaba wa chakula.

Kanali Laban alitumia fursa  hiyo kuzuia matumizi ya mazao ya mahindi,muhogo na mpunga kutengeneza pombe kwa sababu kuna hatari ya kutokea kwa upungufu mkubwa wa chakula.

Aidha,amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nyasa Jimson Mhagama kuhakikisha anatekeleza na kukamilisha miradi yote ya maendeleo waliyoipanga katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Kanali Laban,amehaidi kupambana na watu wanaojihusisha na uvuvi haramu kwenye ziwa nyasa na wanaovua samaki wachanga ambao hawaruhusiwi kisheria kwa kuwa tabia hiyo inachangia sana kuadimika kwa samaki katika ziwa hilo.

Kuhusu sensa ya watu na makazi, Kanali Laban amewaomba wakazi wa wilaya hiyo kujitokeza kushiriki na kutoa ushirikiano kwa makarani watakaofika katika maeneo yao kwa ajili ya kupata taarifa zao na takwimu sahihi zitakazo wezesha Taifa kupanga mipango yake ya maendeleo.

Amewaasa kutoa taarifa zote muhimu na  kwa makarani wa sensa,kuacha kuwaficha watu wenye ulemavu hasa watoto wadogo kwani kufanya hivyo ni kosa na hawatawatendea haki watoto wenye ulemavu.

Mkuu wa mkoa,amewashukuru wananchi  na viongozi wa wilaya ya Nyasa kwa kumpa ushirikiano mkubwa wakati akiwa Mkuu wa wilaya hiyo kwa muda wa mwaka mmoja na miezi tisa na kuhaidi ataendelea kushirikiana nao katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Awali Mbunge wa Jimbo la Nyasa Stella Manyanya, ameiomba serikali kusimamia suala la uvuvi wa samaki wachanga wanaovuliwa katika ziwa hilo kwani tabia hiyo imesababisha samaki kupungua na umaskini mkubwa kwa wananchi wa Nyasa.



Kwa mujibu wa Manyanya,licha ya wilaya hiyo kuwa na utajiri mkubwa wa ziwa maarufu la Nyasa lenye samaki wa aina mbalimbali wakiwamo wa mapambo,hata hivyo ziwa hilo  bado halijawanufaisha wananchi  ambao wanakabiliwa na maisha duni.

Akizungumzia  zoezi la sensa Manyanya alisema,wana Nyasa wana kiu kubwa ya maendeleo kwa hiyo ni muhimu kwao kushiriki kikamilifu zoezi ili kuisaidia serikali  iweze kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo.Alisema,serikali imeshatimiza wajibu wake kwa wananchi wa wilaya hiyo baada ya kukamilisha ujenzi wa Barabara ya lami kutoka Mbinga hadi Mbambabay,kuimarisha Bandari ya Nyasa na kuleta meli za mizigo na abiria zinazofanya safari zake kati ya Nyasa mkoani Ruvuma na Kyela Mbeya.

MWISHO.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.