• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma aweka jiwe la msingi ofisi ya TFS Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: November 19th, 2022

SERIKALI imetoa zaidi ya shilingi milioni 968 kujenga ofisi na nyumba tatu za watumishi katika shamba la miti Mpepo linalohudumiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  wilayani Nyasa mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Mhifadhi Mkuu  wa Shamba la Miti Mpepo John Kimolo amesema mradi wa ujenzi unatekelezwa na Shirika la Nyumba NHC na kwamba jumla ya majengo manne yanajengwa ikiwemo Ofisi kuu ya shamba,nyumba ya Mhifadhi na nyumba mbili za watumishi.

Kimolo amesema serikali inatekeleza mradi huo kwa lengo la kuboresha mazingira bora ya kufanyia kazi na kuishi watumishi wa umma na kwamba mradi umefikia zaidi ya asilimia 95 ya utekelezaji.

“Lengo letu ni kuhamia Mpepo muda wowote,miundombinu ya mtandao wa intaneti na umeme vitakapokamilika kwa sababu shughuli za kiofisi zinahitaji mawasiliano ya mtandao’’,alisisitiza.

Hata hivyo amezitaja changamoto zinazoikabili ofisi hiyo kuwa ni ubovu wa barabara kutoka Nyoni hadi Mpepo inayopitika kwa shida hasa kipindi cha masika,ukosefu wa umeme na moto wa mara kwa mara hasa kipindi cha kiangazi unaosababishwa na wananchi wanapoandaa mashamba yao.

Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi huo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema serikali kupitia Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Ruvuma ukiwemo ujenzi wa  ofisi  za kisasa katika shamba la Mpepo.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amewaonya wananchi kuacha kuharibu mazingira kwa kuchoma moto na kuharibu mazingira kwenye vyanzo vya maji ambavyo amesema vinasababisha mabadiliko ya tabianchi.

Amewaagiza viongozi katika ngazi zote kusimamia  na kuunda Kamati za Mazingira kwenye vijiji ili kuhakikisha kuwa hakuna mtu anayechoma moto misitu na amewataka wananchi kuacha tabia ya kuandaa mashamba kwa kuchoma moto.

“Sisi ndiyo tunaochoma moto na kuharibu vyanzo vya maji,lakini sheria inasema kwenye vyanzo vyote vya maji ndani ya mita 60 hakuna shughuli yeyote ya kibinadamu  inayotakiwa kufanyika,kuanzia sasa ni marufuku kulima au kufanya shughuli zozote kwenye vyanzo vya maji’’,alisisitiza.

Shamba la miti Mpepo ni miongoni mwa mashamba 24 ya miti yanayosimamiwa na kuhudumiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Imeandikwa na Albano Midelo

Kitengo cha Mawasiliano Serikali Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Novemba 19,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.