• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya aagiza watumishi wa umma kumasaidia Rais kutatua kero

Imewekwa kuanzia tarehe: August 26th, 2022


MKUU wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Julius Mtatiro,amewataka watumishi wa umma wilayani humo kufanya kazi kwa weledi,ufanisi ,kuzingatia taratibu na kanuni zilizopo kwa mujibu wa sheria ili kumrahisishia Rais Samia Suluhu  Hassan baadhi ya  majukumu na  kazi ya  kuwahudumi  Watanzania.

Mtatiro ametoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na watumishi wa idara mbalimbali wa Halmashauri ya wilaya Tunduru katika  cha kazi kilichofanyika katika ukumbi mdogo uliopo ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji  mjini Tunduru.
Amewahimiza watumishi wa Halmashauri ya wilaya Tunduru wakiongozwa na wakuu wao wa idara, kuwa wabunifu  sehemu za kazi wanapotekeleza  majukumu yao,ikiwamo kuongeza kasi ya kukusanya mapato ya ndani na kudhibiti mianya ya uvujaji wa mapato ili yaweze kuwahudumia wananchi.

“Mkuu wa idara anayesubiri fedha za sensa zifike na kuzigawa na baadaye anarudi ofisini badala ya kuumiza kichwa kutafuta vyanzo vya mapato huyo hafai kuwa kiongozi”alisema.

Kwa mujibu wa Mtatiro, mtu wa aina hiyo kimsingi ameshindwa kutimiza wajibu wake,kwa sababu sifa ya kiongozi lazima awe mfano kwa kutoa ushauri nini kifanyike kwenye idara yake.

“CMT nendeni mkafanye kazi ya kumsaidia  Rais wetu kutekeleza majukumu yake,tukishindwa kukusanya  na kusimamia mapato tunayokusanya ni dhahiri hatuna msaada wowote katika kumsaidia Mheshimiwa Rais Samia”alisema Mtatiro.

Alisema,mkuu wa idara atakayeshindwa kusimamia na  kuibua vyanzo vipya vya mapato huyo hafai kuongoza idara na atakuwa hatendi haki kwa Rais wetu na wananchi katika wilaya hiyo.

Katika hatua nyingine Mtatiro ameagiza vibanda vyote vinavyomilikiwa na Halmashauri vilivyopo eneo  la stendi ya mabasi Tunduru mjini ambavyo hadi sasa havina wapangaji wapewe watu wenye mahitaji ambao watakuwa tayari kulipa pango na kodi mbalimbali za serikali.

Ametolea mfano baadhi ya vibanda vimepangishwa kwa Sh.30,000 lakini  wapangaji hao wamewapangisha watu wengine kwa gharama  kati ya Sh.150,000 hadi 200,000 kwa mwezi hivyo Halmashauri kukosa mapato makubwa badala yake  watu wachache ndiyo wanaonufaika na uwekezaji huo.

Aidha,amewapongeza watumishi wa Halmashauri  wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Chiza Marando kwa utendaji mzuri wa kazi na ushirikiano hali iliyosaidia shughuli nyingi za serikali kufanyika kwa wakati na ubora wa hali ya juu licha ya ukubwa wa eneo la wilaya hiyo.

Hata hivyo Mtatiro,amewaasa watumishi wote wa serikali katika wilaya hiyo kuacha kufanya kazi kwa mazoea,badala yake kuanza kubadilika katika utekelezaji na utendaji wa kazi zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Tunduru Chiza Marando ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuipatia fedha wilaya hiyo kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alisema,katika kipindi cha mwaka mmoja Serikali imetoa fedha nyingi ambazo zimepelekwa kuboresha sekta ya afya,elimu na maeneo muhimu ya kipaumbele kwa ajili ya kuharakikisha kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja,wilaya na Taifa.

MWISHO




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.