• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa wilaya Namtumbo aagiza kupanda miti kwenye vyanzo vya maji

Imewekwa kuanzia tarehe: March 21st, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma  Mheshimiwa Ngollo Ng’waniduhu Malenya  aliiagiza jumuiya ya watumia maji ya Likuyu na Mandela  kuhakikisha wanaendelea kupanda miti  na kuitunza ili kulinda mazingira ya chanzo hicho kisiharibiwe.

Akiongea  na viongozi wa Jumuiya ya watumia maji wa Likuyuseka na Mandela  pamoja  na wataalamu kutoka Wakala  wa  Maji safi na usafi wa  Mazingira vijijini(RUWASA)  katika chanzo cha mto Namambigi na kusema kuwa chanzo cha mto Namambigi kinatakiwa kipandwe miti ya kutosha na kuitunza ili isife kwa kuwa chanzo hicho ndicho kinachotumika kusambaza maji katika kijiji cha Likuyuseka  na Mandela.

Mkuu wa wilaya alikagua chanzo cha mto Namambigi na kukagua  upandaji wa miti uliofanywa siku za nyuma na kubaini baadhi ya miti imekufa  kwa kukosa uangalizi na kuiagiza jumuiya ya watumia maji kuhakikisha miti inayopandwa katika chanzo hicho inaangaliwa kwa karibu na kutunzwa.

Aidha Malenya alidai miti inayopandwa katika chanzo hicho inanunuliwa kwa shilingi 1000 kila mmoja ,hivyo kuiacha miti iliyopandwa bila uangalizi na kusababisha miti mingine kufa ni kupoteza fedha ,kupoteza muda lakini pia kupoteza mafuta yanayotumika kwenye magari .

Mjumbe wa bodi ya jumuiya ya watumia maji kijiji cha Likuyuseka na Mandela ,diwani wa kata ya Likuyu na makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo kassim Gunda alikiri miti mingine iliyopandwa kufa kwa kukosa uangalizi wa karibu kutoka kwenye uongozi wa jumuiya  kwa kuwa miti hiyo ilipandwa nyakati za kiangazi na uangalizi wa mara kwa mara ulikosekana .

Meneja  kutoka wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini(RUWASA) David Mkondya alimwambia mkuu wa wilaya huyo kuwa usimamizi wa chanzo hicho ulikuwa unafanywa na jumuiya ya watumia maji na kutokana na hali hiyo wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini( RUWASA) itashirikiana na viongozi wa jumuiya katika kusimamia upandaji na utunzaji wa chanzo hicho

Wananchi wa kijiji cha Likuyuseka na Mandela kwa miaka mingi walikuwa wakilalamikia upatikanaji wa maji lakini kwa sasa serikali imejenga mradi mkubwa wa  maji ya mtiririko na kuondoa kero ya upatikanaji wa maji na mto Namambigi maji yake hutumika kusambazwa  katika vijiji hivyo viwili.

Mkuuwa wilaya huyo pamoja na wananchi na wataalamu walipanda miti 70 kwa siku hiyo wakati awamu mbili tofauti  zilipanda miti 120 na miti 630 na kufanya jumla ya miti 820 iliyopandwa katika chanzo hicho  huku miti 120 kati ya miti hiyo ilibainika imekufa kwa kukosa uangalizi wa karibu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.