• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya ya Nyasa atembelea sekondari iliyofaulisha kidato cha sita kwa asilimia 100

Imewekwa kuanzia tarehe: August 25th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabela Chilumba  leo amefanya ziara ya kikazi katika Shule ya Sekondari ya Limbo, iliyopo Kata ya Kilosa, na Shule ya Sekondari ya Mbamba bay Iliyopo, Kata ya Mbamba bay wilayani hapa.

 Matokeo ya Kidato cha sita katika Wilaya ya nyasa 2020,wanafunzi wamefaulu kwa asilimia 100 kwa shule zote Mbambabay Sec. Na St. Pauls' Sec.

Mbambabay: Div I->53, II->88, III->13, ->: 0, O->0.

ST. PAULS: I->13, II->45, III->19, IV->0, O->0. Shule zote ufaulu wa 100%

Ziara hiyo ina  lengo la kutatua changamoto katika shule zote za Sekondari Wilayani hapa,  ili kuongeza Ufaulu wa wanafunzi wa Kidato Cha Nne na kuwapongeza Walimu wa Sekondari ya Mbamba bay, kwa kufaulisha vizuri wanafunzi wa Kidato cha Sita.

Bi Chilumba amefafanua kuwa anachohitaji ni kuona wanafunzi wa Kidato cha nne wanafaulu kama wale wa kidato cha sita kwa kuwa walimu ni hao hao.  

Akiongea na Walimu wa Limbo Sekondari,  amewataka kufanya kazi kwa kufuata maadili ya kazi , na kuwafundisha wanafunzi kwa Upendo na kuwafuatilia,  Shuleni na Nyumbani, na kuwapa mazoezi ya mara kwa mara, ili waweze kujisomea na kujifunza wawapo shuleni na Nyumbani ili kuongeza ari ya  kujifunza.

Ametoa wito kwa Walimu wa Shule hiyo kufundisha kwa bidii na kuacha visingizio mbalimbali, kwa kuwa wao kama wataalamu wa elimu wamepelekwa mashuleni ili kuwafundisha wanafunzi , wazazi, na wanajamii kutatua changamoto ili kuleta mabadiliko katika maeneo yao ya Kazi.

Aidha amewaagiza wakaguzi wa Elimu Wilayani Nyasa kupeleka nakala ya Taarifa ya ukaguzi na kusema kuwa,  hatawavumilia walimu wazembe,  ambao hawatafaulisha kwa kuwa malengo ya kila mwalimu ni kuhakikisha wanafunzi wake wanafaulu masomo anayofundisha na kamwe hatamvumilia mwalimu mzembe

“Nawaagiza walimu wakuu na wakaguzi wa elimu wilayani hapa kwamba, hamtakiwi kuwavumilia walimu wazembe ambao hawafaulishi, kazi yao ni kutoa visingizio, hatuwezi kufikia hapo tunatakiwa kubadilika, na kuhakikisha wanafunzi wanafaulu kwa kila masomo yenu  mnayofundisha. Lakini pia tunatakiwa kuwa na malengo ya kuhakikisha kuwa wanafunzi wanafaulu kwa hali yoyote ile”.Alisema Chilumba.

Katika shule ya Sekondari ya Mbamba Bay Amewapongeza walimu wa Shule hiyo kwa kufaulisha wanafuzi wote wa Kidato cha sita na kuwataka matokeo kama hayo yapatikane kidato cha nne, na mbinu walizotumia kufundisha Kidato cha sita wazitumie kufaulisha Kidato cha nne.

Aidha amewashuru na kuwapongeza wananchi wa Wilaya ya Nyasa,  kupitia ukurasa wa kijamii wa Facebook wa  Nyasa kwetu Forum kwa kufuatilia habari za Nyasa na kuchangia kwa umakini mada zinazohusu uboreshaji wa Elimu, miundombinu,na masuala mengine ya Kijamii  Kwa Wilaya ya Nyasa.

Awali walimu hao walizitaja changamoto wanazokutana nazo ni pamoja na Kutopata ushirikiano na wazazi,  kwa kuwahamasisha wanafunzi kusoma ,kutochangia chakula na kuwafanya wanafunzi kusoma na njaa, kutembea umbali mrefu na kufika shule wakiwa wamechoka na kutomudu masomo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa bw. Jimson Mhagama aliwataka walimu kuhakikisha wanafundisha na kuhakikisha wanafunzi wanafaulu ili kufikia malengo ya Wilaya ya kufaulisha wanafunzi wote wa Kidato cha Nne, kwa kutoa Elimu kwa wazazi na walezi kwa kuwa wazazi wengine hawana ufahamu juu ya kutoa ushirikiano kwa walimu ili kuinua kiwango cha Elimu Wilayani Nyasa.

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa katika ziara hiyo aliambatana na Kamati ya Ulizi na Usalama Wilaya ya Nyasa.Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nyasa na Wakuu wa Idara za Elimu Sekondari,Elimu Msingi, Tume ya Utumishi wa Walimu, na Mkuu wa Idara ya Utawala na Raslimali Watu Bw.Liston Moyo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.