• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya ya Songea awafunda wanafunzi

Imewekwa kuanzia tarehe: November 2nd, 2022

MKUU wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma Pololet Mgema,amewataka wanafunzi wa kidato cha nne shule ya Sekondari Mkombozi,kutumia siku chache zilizobaki kusoma kwa bidii na kujikumbusha waliyofundishwa na walimu wao ili waweze kufanya vema katika mitihani ya Taifa inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni nchini kote.

Mgema ametoa wito huo jana,wakati akizungumza na wanafunzi,walimu na wazazi kwenye mahafali ya pili ya kidato cha nne ambapo jumla ya wanafunzi 39 wanarajiwa kumaliza masomo yao siku chache zijazo..

Aidha,amewaonya kwenda kujiepusha na tabia ya ulevi,ndoa za mapema na ngono uzembe ambazo  ni chanzo cha kupata magonjwa hatari ikiwamo ukimwi, na kukatisha ndoto zao.

Mgema ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo,ametoa onya kali kwa watu wazima kujiepusha kufanya mapenzi na wanafunzi ili kuepuka mikono ya sheria.

Badala yake,amewataka kuwa walinzi wa watoto hao ili wafanikiwe katika safari yao na hatimaye wawe viongozi bora watakao litumikia Taifa katika nyanja mbalimbali.

Amempongeza Mkurugenzi wa shule hiyo Franco Komba  kutokana na jitihada zake za kuongeza miundombinu ya shule ambayo imewezesha kuwa na mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia, hata hivyo ameshauri  kutafuta walimu wazuri hasa wa masomo ya Sayansi ambao watakuwa chachu ya kuongezeka kwa taaluma katika shule hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo Fidelis Komba,amewapongeza wahitimu hao kwa uvumilifu wao katika kipindi chote cha miaka minne,kwa kuwa walikutana na chagamoto mbalimbali wakati wa safari yao ya masomo.

Komba amewaasa vijana hao wanaotarajiwa kuhitimu kidato cha nne siku chache zijazo,kujiandaa vema na mitihani kwa kumshirikisha Mungu kwa kila jambo ikiwamo kufanya maombi ya mara kwa mara ili aweze kuwaongoza na kuwapa uwezo katika kujibu kwa usahihi maswali ya mitihani yao.

Hata hivyo amewakumbusha wanaporudi nyumbani,wakawe na maadili mema,kuwaheshimu wazazi na jamii inayowazunguka na kuheshimu sheria za nchi kama walivyokuwa wakiishi shuleni na siyo kwenda kuwa watu wa onyo na kukosa msaada wa jamii.

Katika  hatua nyingine Komba,amewataka kuwa mfano bora na kwenda kuwasaidia wazazi wao kazi mbalimbali ili kuongeza kipato,badala ya kwenda kuwa mizigo isiyokuwa na faida  kwa familia zao.

“wazazi msiwaache hawa watoto nyumbani mnapokwenda kwenye kazi za uzalishaji mali,nawaombeni sana muwe  nao pamoja ili kuwafundisha kazi kama sehemu ya kujiandaa waweze kujitegemea watakapo kuwa watu wazima”alisema Mwalimu Komba.

Naye Mwalimu wa taaluma Jacob Kauzeni alisema,hayo ni mahafali ya pili ya kidato cha nne ambapo mwaka jana  jumla ya wanafunzi 40 walihitimu masomo yao na kati ya hao wanafunzi sita daraja la1, wanafunzi kumi na sita walipata daraja la 2,wanafunzi kumi na nne walipata daraja la 3 na wanafunzi  wa nne walipata daraja la nne na hakuna mwanafunzi aliyefeli.


Alisema, katika matokeo hayo wanafunzi wote walichaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na baadhi yao walipata nafasi ya kujiunga na vyuo mbalimbali hapa nchini.

Awali katika risala yao iliyosomwa na Jenifar Ndenga wahitimu hao,wamewapongeza walimu na mmiliki wa shule  kuwapatia misingi imara itakayowawezesha kuwa na uwezo wa kujitegemea katika maisha yao.

Ndege alisema, hiyo ina miundombinu na mahitaji yote muhimu inayopaswa kuwepo kwa ajili ya wanafunzi wanaoishi bweni na wale wanaotoka nyumbani.Wameiomba Serikali kuisaidia shule hiyo kumaliza tatizo la maji,kwani sasa wanatumia  maji ya kisima ambacho hakitoshelezi mahitaji ya wanafunzi waliopo na wakati mwingine wanalazimika kutumia vyanzo visivyo rasmi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.