• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MNADA wa kwanza wa korosho wafanyika Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: October 25th, 2024

WAKULIMA wa zao la korosho mkoani Ruvuma,wameuza jumla ya kilo  milioni 1,248,620 kwa bei ya Sh.3,245 kwa kilo moja katika mnada wa kwanza uliofanyika katika Chama cha msingi cha Namitili kijiji cha Nakapanya kata ya Nakapanya.

Meneja Mkuu wa Chama kikuu cha Ushirika wilaya ya Tunduru(Tamcu)Marcelino Mrope alisema,katika msimu kilimo 2024/2025 malengo ni  kukusanya na kuuza tani 28,000 ambazo ni zaidi ya tani 1,937 zilizokusanywa katika msimu wa kilimo 2023/2024.

Alisema,kati ya tani hizo wakulima wa mkoa wa Ruvuma wanatarajia kukusanya tani 27,950 na tani 50 zitakusanywa kutoka kwa wakulima wa mikoa mingine ikiwemo Njombe hasa wilaya ya Ludewa ambao wanahudumiwa na Chama kikuu cha Ushirika Tamcu.

Mrope alisema,katika msimu mauzo msimu wa 2024/2025 Tamcu itaendelea kutumia mfumo wa mauzo wa kimtandao(Online Trading System)unaosimamiwa na taasisi za ya Serikali ya soko la bidhaa Tanzania(TMX).

Aidha,katika msimu wa mauzo 2023/2024 jumla ya kilo 26,062,323 zilikusanywa na kuuzwa katika maghala makuu manane yaliyopewa kibali na bodi ya stakabadhi ghala ambapo uzalishaji uliongezeka ukilinganisha na msimu 2022/2023 ambapo kilo 15,317,972 zilikusanywa na kuuzwa ikiwa ni ongezeko la kilo 10,744,351 sawa na asilimia 70.1.

Alisema,katika msimu 2023/2024 korosho ziliuzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghala kupitia minada na bei ilikuwa Sh.2,015  hadi Sh.1,345.

Alieleza kuwa,pamoja na mafanikio yaliyopatikana hata hivyo kulikuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya Amcos kutozingatia mwongozo unaotaka kupokea korosho zenye ubora katika maghala,kuwepo kwa maghala manane ambayo ni mengi badala ya matatu kama ilivyokuwa msimu 2021/2022 na sita ya msimu 2022/2023.

Kwa mujibu wa Mrope,kuwepo kwa maghala mengi kumesababisha watunza maghala kutozingatia ubora wakati wa kupokea korosho, hivyo kusababisha korosho kushuka ubora wake.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas,amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na nzuri ya kusimamia sekta ya kilimo hapa nchini  ambapo mkoa wa Ruvuma ni wanufaika wakubwa.

Ahmed alisema,katika msimu 2023/2024 changamoto kubwa ilikuwa kuchelewa kwa malipo ya wakulima,kukosekana kwa taarifa sahihi za uzalishaji(kanzi data)uzalishaji hafifu wa korosho,utoroshaji wa korosho,upotevu wa mazao na kukosekana kwa huduma za ugani kwa wakulima.

Amewataka wakulima kuendelea kuuza korosho zao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na kusisitiza malipo lazima yafanyike kupitia  Chama kikuu cha Ushirika badala ya vyama vya msingi vya ushirika(Amcos).

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Simon Chacha alisema,wilaya ya Tunduru ni wazalishaji wakubwa wa zao  la korosho katika mkoa wa Ruvuma na amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa pembejeo za ruzuku kwa wakulima wa zao la korosho.

Chacha amewataka watendaji wa vyama vya msingi vya ushirika(Amcos) na Chama kikuu(Tamcu)kuhakikisha wanatekeleza maagizo ya Serikali yanayotaka fedha za wakulima kulipwa kwa wakati na kutumia mizani za Kidigitali kwenye kupima korosho na mazao mengine yanayouzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuepusha malalamiko kwa wakulima.

Mkurugenzi wa Bodi ya korosho Tanzania Francis Alfredy alisema,huo ni mnada wa kwanza wa korosho katika mkoa wa Ruvuma na minada kama hiyo imeshafanyika katika mkoa wa Mtwara na bei ilikuwa Sh.4,195 kwa kilo moja.

Alisema,mwenendo wa bei ya korosho katika soko la Dunia ilitegemewa kuwa kati ya Sh.3,000 hadi 3,600  kwa kilo moja,lakini jambo la kufurahisha bei ilipanda hadi kufikia Sh.4.000.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.