• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MNADA wa kwanza wa ufuta Tunduru waingiza bilioni tatu

Imewekwa kuanzia tarehe: June 6th, 2023

WAKULIMA wa kijiji cha Lukumbule Halmashauri ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma,wameuza kilo 857,977.70 za ufuta zenye thamani ya Sh.bilioni 3,279,252,792.70 katika mnada wa kwanza uliofanyika katika viwanja vya Chama Kikuu cha msingi  Nguvumali.

Katika mnada huo jumla ya makampuni 14 yalijitokeza kuomba kununua ufuta ambapo kampuni tatu za Yihayikerry Hysease,Mohamed Enterprises na Lenic Tanzania zilishinda  baada ya kuomba kununua kwa bei ya wastani wa Sh.3,822 kwa kilo.

Akizungumza katika mnada huo Mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro, amesisitiza suala la wakulima kuuza ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani ulioonyesha mafanikio makubwa kwao,na kukataa kuuza kwa wafanya biashara wauni wanaopita mashambani ili kununua kwa bei ndogo.

Mtatiro,amewataka wanunuzi kuongeza bei ili kuwahamasisha wakulima kuongeza uzalishaji wa zao hilo mashambani,hatua ambayo itawasaidia kupata ufuta mwingi utakao zalishwa na wakulima kupitia vyama vyao vya msingi vya ushirika(Amcos).

Aidha amewahakikishia wakulima kuwa,Serikali haitachukua ela ya mkulima yoyote wa ufuta na mazao mengine yatakayozalishwa, na fedha zote zitakwenda kwa wakulima ili waweze kufaidika na nguvu zao kupitia shughuli zao za kilimo na uuzaji wa mazao yao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

Mtatiro alisema,badala yake serikali itaendelea kusimamia soko la mazao na tozo zilizopo kisheria ambazo haziwaumizi wakulima na kuwaonya wafanyabiashara wanaotaka kununua ufuta na mazao mengine ya wakulima kuzingatia sheria na kufuata utaratibu uliowekwa na serikali.

Pia,amewakumbusha wananchi kuhakikisha wanajiwekea akiba ya chakula kwa ajili ya familia zao na kuepuka tamaa ya kuuza chakula chote ili kupata fedha na umuhimu wa kuchangia chakula kwa watoto wao waliopo shuleni.

Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika wilayani humo Tamcu Ltd Mussa Manjaule,amewapongeza wakulima  hao kutokana na uzalishaji mkubwa wa zao la ufuta katika msimu wa kilimo wa 2022/2023.

Manjaule alisema,wananchi wa kijiji hicho wamekuwa wazalishaji wakubwa wa ufuta kila mwaka licha ya kukutana na changamoto mbalimbali na kuwataka wakulima wa maeneo mengine kwenda kujifunza kwa wenzao wa Lukumbule.

Awali Meneja Shughuli wa Tamcu Marcelino Mrope alisema,kuelekea msimu wa ufuta 2023/2024 Chama kikuu cha Ushirika Tunduru(Tamcu Ltd) kinarajia kukusanya ufuta kilo milioni 3,822,561 ikiwa ni zaidi ya kilo milioni1,273,746 kutoka  kilo 2,548,815 ambazo zilizalishwa katika msimu 2022/2023.

Mrope alisema, katika msimu wa masoko wa mazao ya kilimo 2023/2024 Serikali imetoa mwongozo wa matumizi ya mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mazao ya ufuta,mbaazi, soya na korosho na Tamcu itaendelea kusimamia sheria na kutekeleza mwongozo huo mwa maslahi mapana kwa wakulima.

Aidha alieleza kuwa,wakulima wameendelea kufurahia mfumo huo kwa kuwa, una manufaa na faida kubwa kwao baada ya bei ya mazao yanayouzwa kupitia stakabadhi ghalani kupanda mwaka hadi mwaka ikilinganishwa na mfumo wa soko huria.

Baadhi ya wakulima wa kijiji hicho,wameishukuru serikali ya awamu ya sita kuendelea kusimamia soko la ufuta na mazao mengine kutokana na kupanda thamani na hivyo kufanikiwa kuwa na soko la uhakika na kupata bei nzuri.

Malaje Daud alisema kabla ya kuanza kwa mfumo huo miaka mitatu iliyopita ,bei ya mazao ilikuwa chini tofauti na sasa ambapo kupitia mfumo huo bei ya mazao yao imekuwa kubwa  na hivyo wakulima wengi kuona kilimo kina manufaa makubwa.

Hata hivyo,ameiomba serikali iendelea kuwabana wanunuzi  kwa kuongeze bei ya kununua mazao ili kuwahamasisha wakulima waendelee kuzalisha kwa wingi na minada hiyo ifanyike katika vijiji vyenye uzalishaji mkubwa.

Fenis Soka alisema,amefurahishwa na ongezeko la bei ya ufuta ikilinganishwa na mwaka jana,lakini ameiomba serikali kuhakikisha inawadhibiti wanyama wakali na waharibifu wanaoharibu na kula mazao mashambani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.