• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MNDEME aitaka jamii kuacha ukatili wa kijinsia

Imewekwa kuanzia tarehe: March 10th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christine Mndeme, ameitaka jamii kuacha ukatili wa kijinsia, na wahamasike  kuongeza fursa za Kiuchumi kwa Wanawake kwa kuwajengea  uwezo wa kitaalam, kibiashara, na mbinu za kupata mtaji na masoko.

Aliyasema hayo jana wakati akihutubia mamia ya wanawake, katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani kimkoa yaliyofanyika katika Viwanja vya Polisi ,Mjini Mbamba-bay Wilayani hapa.

Mndeme aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabela Chilumba, alifafanua kuwa, jamii inatakiwa kuacha mara moja Ukatili wa kijinsia, na badala yake wahamasike kuongeza fursa za kiuchumi kwa wanawake,kwa kuwajengea uwezo wa kitaalam, kibiashara, na mbinu za kupata mtaji wa masoko ili waondokane na utegemezi.

Aliongeza kuwa,  Serikali na wadau kwa ngazi zote, haina budi kuendelea kuweka vipaumbele vya kuwainua Wanawake  Vijijini, ili waweze kuwa Wajasiliamali wenye bidhaa bora na kuwatafutia masoko ya Kimataifa kwa lengo la kuitangaza nchi yetu, na kuinua uchumi wa Taifa letu.

“jamii haina budi kuongeza fursa za Kiuchumi kwa Wanawake ili kuwajengea uwezo wa kitaalam, kibiashara, mbinu za kupata mtaji na masoko. Serikali na wadau na ngazi zote kuendendelea kuweka vipaumbele vya kuwainua Wanawake  Vijijini waweze kuwa Wajasiliamali wenye bidhaa bora na kuwatafutia masoko ya Kimataifa kwa lengo la kuitangaza nchi yetu lakini vilevile kuinua uchumi wa Taifa letu.

 

Naye mkuu wa Idara ya maendeleo ya Jamii Mkoa wa Ruvuma Bi Zawadi Nyoni , akitoa maelezo ya idara yake alisema , amewahamasisha wanawake wengi kujiunga na kuanzisha vikundi vya wanawake ili kuvipatia mikopo mbalimbali, na hadi Desemba 2019 jumla ya vikundi vya wanawake 389 vimeundwa na kukopeshwa tsh 509,174,487.00 ikiwa ni fedha za asilimia kumi za mapato ya ndani za Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma.

Bi Nyoni aliongeza kuwa idara yake inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa watumishi wa idara ya maendeleo ya jamii, uhaba wa vitendea kazi ikiwemo usafiri, kutopewa fedha za asilimia kumi kwa wakati na hata zikipatikana hazikidhi mahitaji ya waombaji wa mikopo.

Maadhimisho hayo yameambatana na shughuli mbalimbali zilizofanyika Wilayani hapa, ikiwa ni pamoja na Kongamano la Wanawake wajasiliamali ambapo walipewa elimu ya ujasiliamali na elimu ya kuzifahamu haki na Sheria za ndoa na Mirathi, pamoja na kutembelea na kutoa misaada mbalimbali katika wodi ya wazazi (Maternity) katika kituo cha afya cha Mbamba-bay Wilayani Nyasa.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni sabuni ya unga mifuko mitatu,buti pea tisa, sabuni za mche katoni tatu, mpira ya kutandika kitandani meta nane, brash za kufanyia usafi 6, Ndoo za taka 06, ndoo za kudekia 04.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.