• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MRADI mkubwa utakaomaliza kero ya maji Manispaa ya Songea unakuja

Imewekwa kuanzia tarehe: March 15th, 2021


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema serikali inakwenda kutekeleza mradi mkubwa unaofadhiliwa na nchi ya India ambao unakwenda kumaliza kero ya maji katika Manispaa ya Songea.

Akizungumza ofisini kwake kuelekea maadhimisho ya wiki ya maji inayoanza Machi 16 hadi 22 mwaka huu,Mndeme amesema mradi huo unaofadhiliwa na serikali ya India unagharimu zaidi ya Dola za Marekani milioni 45.3.

“Kinachoendelea hivi sasa kupitia Wizara yetu ya Maji,ni hatua za manunuzi ya wakandarasi wa kutekeleza mradi huo mkubwa ambao utahusisha ujenzi wa bwawa la kuhifadhia maji ambalo litakuwa na uwezo wa kuhifadhi maji lita bilioni tano’’,alisema Mndeme.

Amesema mradi huo pia utahusisha upanuzi wa mtambo wa  kusafisha maji na kutibu maji safi  zaidi ya lita milioni 51.4 kwa siku,ujenzi wa matanki manne ya kuhifadhi maji yenye uwezo wa lita milioni 18.2 na ulazaji wa mabomba yenye uwezo wa kusafirisha maji kilometa 190.3.

Mndeme amesema mradi huo utakapokamilika zaidi ya asilimia 95 ya wakazi wa Manispaa ya Songea watakuwa wanapata huduma ya maji safi na salama.

Amesema wananchi wa Manispaa ya Songea ambao hawajafikiwa na huduma ya maji,kupitia mradi huu mkubwa watapata maji na kuwezesha asilimia ya usambazaji maji kwenye manispaa hiyo kuongezeka toka asilimia 86.2 hadi 95 na kwamba lengo ni kufikia asilimia 100 ya kutoa maji katika miji ya Songea,Tunduru na Mbinga.

Hata hivyo amesema katika miji ya Mbinga na Tunduru serikali inatenga fedha kwenye bajeti ya kila mwaka kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya usambazaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Kwa upande wake Meneja wa  RUWASA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman  Ganshonga amesema ili miundombinu ya maji iwe endelevu, wananchi wanatakiwa kuilinda miundombinu na kuvitunza vyanzo vya maji kwa sababu serikali inawekeza fedha nyingi kwenye miradi hiyo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 15,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.