• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MRADI wa miti kuwaingiza chama kikuu cha Ushirika MBIFACU milioni 553

Imewekwa kuanzia tarehe: July 10th, 2020

CHAMA Kikuu cha Ushirika  cha Wilaya za Mbinga na Nyasa(MBIFACU)  kimeanzisha shamba la miti la Kitelea mjini Mbinga  lenye ukubwa wa hekari 39 lililopo kando kando ya barabara iendayo Mbambabay wilayani Nyasa.

Kaimu Meneja wa MBIFACU Henrick Ndimbo  amesema chama hicho kimeanzisha shamba hilo kwa lengo la kujiongezea mapato na kuimarisha ushirika kutokana na maelekezo ya serikali ya awamu ya Tano yenye lengo la kufufua ushirika nchini.

Ndimbo amesema kupitia shamba hilo,katika msimu wa mwaka 2019/2020 MBIFACU imefanikiwa kuuza miti 118 yenye thamani ya shilingi 2,360,000/= na kwamba fedha hizo ziliingizwa kwenye mapato ya chama ili kuweza kusaidia uendeshaji wa shughuli mbalimbali za chama.

“Mpango mkakati wa  mwaka 2020/2021 ni uvunaji wa miti kwa hekari 30 na uchanaji wa mbao ambazo zinatarajia kutuingizia kipato cha shilingi milioni 553,630,000/= baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji,ikiwa ni moja ya juhudi za kuongeza mapato ya ndani ya chama ili kiweze kujitegemea’’,alisisitiza Ndimbo.

Ndimbo ametoa rai kwa Taasisi zote kushirikiana na MBIFACU katika kutekeleza na kusimamia mfumo wa ushirika kwa sababu  ndiyo mkombozi wa wakulima ambao unaweza kuwanufaisha wakulima,endapo mfumo  wa ushirika utasimamiwa vizuri kupitia wataalam.

Amesisitiza kuwa ushirika utaongeza uzalishaji kwa kuongeza kipato cha wakulima moja kwa moja na kuongeza mapato ya Halmashauri ya serikali kwa ujumla.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa MBIFACU Winfred Lupembe  amesema shamba la miti la Kitelea ni la miti ya zamani ambapo MBIFACU imeamua kuliboresha shamba hilo kwa kuvuna miti yote kwa matumizi ya mbao na kuni na kwamba baada ya kukamilisha kazi ya kuvuna,MBIFACU inatarajia kupanda miti upya kibiashara na kuingiza mapato makubwa zaidi.

Lupembe amesisitiza kuwa zoezi la uvunaji miti ya zamani na kupanda miti mipya linaendelea ambapo katika eneo hilo tayari imepandwa miti mipya 600 na kwamba shamba la miti linalomilikiwa na MBIFACU,ukitembea  kwa mguu unaweza kutembea kwa saa mbili na nusu kuzunguka shamba lote.

Amesema miti yote ambayo ilipandwa katika shamba la miti la Kitelea ilishavunwa na kwamba miti  iliyopo hivi sasa ni michipukizi ya miti  zamani ambayo pia inavunwa kwa ajili ya mbao za kuendeleza mradi wa ukarabati wa hoteli ya MBICU kuwa katika viwango vya kimataifa.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 11,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.