• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MUONEKANO wa chuo cha VETA Nyasa ,RC Mndeme afanya ukaguzi eneo la mradi

Imewekwa kuanzia tarehe: June 1st, 2020

Mkuu  wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amekagua mradi wa chuo cha VETA Nyasa kinachojengwa katika kijiji cha Ruhekei Kata ya Kilosa Mbambabay kwa gharama ya shilingi bilioni 2.1.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa chuo hicho,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nyasa Jimson Mhagama amesema mradi huo utakuwa na majengo 15 na ulianza Aprili,2020 na unatarajia kukamilika Julai mwaka huu.

Amesema mradi huo unahusisha nyumba za watumishi,hosteli za wanachuo,bwalo la chakula, vyoo,madarasa na karakana na kwamba bati za kutosheleza majengo yote zimeshafika.

 Kwa mujibu wa Mhagama, katika awamu ya kwanza ya ujenzi,serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni moja na kwamba hadi kukamilika kwa mradi huo utagharimu shilingi bilioni 2.1.

“Katika awamu ya kwanza ipo nyumba ya Mkuu wa chuo pekee yake,katika awamu nyingine zitajengwa nyumba za watumishi wengine,huu ni mradi mkubwa wa kwanza kutekelezwa kwa force account katika Halmashauri ya Nyasa’’,alisisitiza Mhagama.

Amesema mradi huo unatekelezwa na SUMA JKT ambapo hadi sasa utekelezaji wake unafanyika vizuri  na kwamba ana matumaini makubwa kwamba utakamilika kwa wakati.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  amemshukuru Rais Dkt John Magufuli kwa kutoa upendeleo maalum katika Mkoa wa Ruvuma,ambao sasa utakuwa na vyuo vya VETA vitatu ikiwemo cha Songea,Namtumbo na sasa chuo cha VETA Nyasa.

“Vyuo cha VETA vimekuwa vinajengwa makao makuu tu ya mikoa,lakini sisi wanaruvuma tumependelewa,wilaya tatu zinaenda kuwa na vyuo vya VETA,Songea na Namtumbo vyuo vinatoa mafunzo’’,alisisitiza Mndeme.

Amesema vyuo hivyo vitakwenda kuzalisha vijana ambao watakuwa na ujuzi mkubwa wa kuajiriwa na kujiajiri hivyo kuchangia kukuza uchumi wa Taifa kupitia fani mbalimbali zikiwemo ushonaji,ujenzi,ufundi magari, kompyuta,upishi na fani nyingine.

Katika Hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewashauri wanaosimamia ujenzi wa  vyuo vya VETA nchini,kufanya michoro ya majengo kwa gharama nafuu,badala ya kutumia michoro inayotumika sasa yenye gharama kubwa na haiendani mazingira ya eneo la ujenzi.

IMEANDIKWA NA ALBANO MIDELO

AFISA HABARI WA MKOA WA RUVUMA

MEI 30,2020

MBAMBA BAY

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.