• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: May 8th, 2025

Jumla ya miradi 76 yenye thamani ya shilingi bilioni 96.8 inatarajiwa kutembelewa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 katika Mkoa wa Ruvuma.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed wakati anazungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea kuhusu mbio maalum za Mwenge wa Uhuru ambao unaanza mbio zake mkoani Ruvuma Mei 9  na kukamilisha Mei16 mwaka huu.

 Amesema miradi hiyo inajumuisha sekta muhimu kama afya, elimu, maji, barabara na huduma nyingine za kijamii na kwamba Kati ya miradi hiyo,miradi 17 itazinduliwa rasmi,miradi13 itawekewa jiwe la msingi  na 33 itakaguliwa ili kuona utekelezaji wake.

Ameongeza kuwa  miradi mingine 13 itahusisha ugawaji wa vifaa mbalimbali kwa wananchi. Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na kwamba miradi hiyo inaonesha dhamira ya Serikali kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi.

Kwa mujibu wa ratiba ya mbio hizo, Mwenge wa Uhuru utakimbizwa kuanzia Mei 9 hadi 16, 2025 katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma kwa umbali wa jumla ya kilomita 1,378.90.

“Mwenge huo utaanza Halmashauri ya Madaba, kupita Songea, Mbinga, Nyasa, Mji wa Mbinga, Manispaa ya Songea, Namtumbo na kumalizia Tunduru’’,alisema Kanali Abbas.

Katika hotuba yake kwa wanahabari, Kanali Ahmed ameutaja ujumbe mkuu wa Mwenge wa Uhuru 2025  kuwa ni “Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa amani na utulivu”, ambao unalenga kuhamasisha wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi mkuu ujao.

Mbali na kauli mbiu kuu hiyo,mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu pia zimejikita katika kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora, mapambano dhidi ya rushwa, VVU/UKIMWIna matumizi ya dawa za kulevya na malaria.

 Kanali Ahmed amebainisha kuwa kampeni hizi zinaendelea kuwa silaha muhimu za kujenga taifa lenye afya, maadili na ustawi wa jamii.

Ametoa rai kwa wananchi wa Ruvuma kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru na kushuhudia hatua za utekelezaji wa miradi yao.

Amesisitiza kuwa Mwenge wa Uhuru si tu ishara ya historia ya uhuru, bali pia chombo cha kuangaza maendeleo, ushirikiano na maandalizi ya uchaguzi wa amani mwaka 2025.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.