• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru ulivyoridhia miradi yote Madaba

Imewekwa kuanzia tarehe: April 28th, 2023

 

MWENGE wa Uhuru Kitaifa 2023 umeendelea na ziara yake katika wilaya ya Songea mkoani Ruvuma ambapo Aprili 19,2023 umekagua na kuridhia miradi yote katika Halmashauri ya Madaba yenye thamani ya shilingi milioni 859

Miongoni mwa miradi iliyoridhiwa na Mwenge wa Uhuru ni mradi wa ujenzi wa maji katika Kijiji cha Mbangamawe ambapo serikali kupitia RUWASA imetoa zaidi ya shilingi milioni 545 kutekeleza mradi huo.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023 ,Meneja wa RUWASA Wilaya ya Songea Mhandisi Mathias Charles amesema mradi huo ukikamilika kwa asilimia 100 utawawezesha wakazi 2,800 kupata maji safi na salama ya bomba.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo,Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023 Ndugu Abdalla Shaib Kaim amewapongeza RUWASA kwa  kuendelea kutekeleza miradi ya maji yenye viwango vinavyoendana na thamani ya fedha zilizotolewa na serikali.

 Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile kwa niaba ya wananchi amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizowezesha kujenga mradi wa maji katika Kijiji cha Mbangmawe ambacho hakijawahi kuwa na maji ya bomba tangu kuanzishwa kwake.Miradi mingine ambayo imetembelewa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Madaba ni mradi wa lishe katika zahanati ya Likarangilo na mradi wa mapambano dhidi ya dawa za kulevya katika Kijiji cha Magingo.

Mwenge wa Uhuru pia ulikagua mradi wa utunzaji mazingira na kutembelea chanzo cha maji katika hifadhi ya misitu ya Wino inayosimamiwa na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS),ambapo Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru amepongeza kazi kubwa inayofanywa na TFS kwenye utunzaji mazingira nchini.

Katika Halmashauri ya Madaba pia Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye mradi wa nyumba ya kulala wageni katika Kijiji cha Lilondo iliyojengwa na Mwananchi binafsi Ibrahimu Kilangwa kwa gharama ya shilingi milioni 126.

Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika Halmashauri ya Madaba pia ameweka jiwe la msingi katika kikundi cha  Kwetu Madaba ambacho kimepewa mkopo na Halmashauri shilingi milioni 44 kufanya mradi wa kufyatua tofali za saruji.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.