• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru waangaza Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: May 15th, 2025

Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake mkoani Ruvuma, umeendelea kuangaza matumaini kwa wananchi kwa kupitia, kuzindua, na kuweka mawe ya msingi katika miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.5 katika Wilaya ya Namtumbo pekee.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2025, Ismail Ali Ussi, amesema ameridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali katika wilaya hiyo, hususan miradi ya maji na elimu ambayo imeelezwa kuwa na ubora wa hali ya juu unaokidhi viwango vya kitaifa.

Mradi wa maji wa bilioni 1.1 kuwaondolea wananchi kero ya maji

Katika hatua kubwa ya mapinduzi ya huduma ya maji safi na salama, Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Msisima unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.1, ambao utahudumia wakazi 4,081 wa vijiji vya Msisima na Mnalawi.

Mhandisi David Mkondya, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo, amesema utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 60, na unatarajiwa kuondoa kabisa tatizo la upatikanaji wa maji safi katika vijiji hivyo.

Madarasa mapya kupunguza msongamano

Mwenge wa Uhuru pia umefungua rasmi mradi wa ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu sita ya vyoo katika Shule ya Msingi Mtakanini, unaotekelezwa kupitia programu ya BOOST kwa gharama ya shilingi milioni 107.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Namtumbo, Philemon Magesa, amesema ujenzi huo unakwenda kupunguza kwa kiasi kikubwa msongamano wa wanafunzi darasani, hali inayoboresha mazingira ya ujifunzaji.

Kituo cha mafuta na vifaa vya afya navyo vafaidika

Katika kuimarisha huduma za kijamii na kiuchumi, Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye kituo cha mafuta cha Anchr Oil Mtwara Pachani kilichopo Kata ya Luegu, kilichogharimu takribani shilingi milioni 160 hadi sasa.

Aidha, Mwenge umekagua vifaa vya kisasa vya meno vikiwemo dental chair na dental X-ray machine vilivyonunuliwa kwa shilingi milioni 18.94 kwa ajili ya Kituo cha Afya Lusewa, fedha zilizotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mkurugenzi Magesa amesema vifaa hivyo ni hatua muhimu katika kuimarisha huduma za afya ya kinywa na meno kwa wakazi wa eneo hilo.

Nishati safi yapelekwa kwa wananchi

Katika jitihada za kuhamasisha matumizi ya nishati safi, Mwenge wa Uhuru umetoa mitungi 20 ya gesi safi yenye thamani ya shilingi milioni moja kwa wananchi wa Namtumbo. Magesa amesema Halmashauri inaendelea kutoa elimu kuhusu nishati safi ili kulinda afya na mazingira.

Kiongozi wa Mwenge atoa pongezi kwa Serikali ya Wilaya

Akihitimisha ziara hiyo, Ismail Ussi ameipongeza Serikali ya Wilaya ya Namtumbo kwa kusimamia vizuri miradi ya kimkakati, hasa miradi ya maji na elimu, akieleza kuwa ni hatua madhubuti za kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amewezesha fedha nyingi kwa ajili ya miradi hiyo.

Amesisitiza kuwa miradi hiyo ni ya mfano na itakuwa na manufaa ya muda mrefu, hivyo wananchi wanapaswa kuithamini na kuitunza.

Mwenge wa Uhuru unaendelea na mbio zake katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma na unatarajiwa kukabidhiwa mkoani Mtwara Mei 17, 2025.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MSIKIMBILIE hasara,serikali inakuja na bei ya neema kwa mahindi Julai

    May 31, 2025
  • WAKULIMA Namtumbo wachuma neema ya ufuta kwa teknlojia mpya ya mnada wa kidigitali

    May 31, 2025
  • RUSHWA yazidi kuporomoka na kukosa nafasi Ruvuma

    May 31, 2025
  • SERIKALI yatoa fidia ya bilioni 2.5 kupisha mradi wa umeme wa Grid Songea-Tunduru

    May 31, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.