• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote nane Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: September 2nd, 2021

MBIO maalum za Mwenge wa uhuru mwaka 2021 zimekubali kuizindua na kuweka mawe ya msingi miradi yote nane katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.2

Kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru mwaka huu Luteni Josephine Mwambashi ameikagua miradi yote kwa kushirikiana na wenzake na kuikubali miradi yote  iliyopangwa kutembelewa na Mwenge wa Uhuru mwaka huu.

Akisoma taarifa ya mradi wa  katika kijiji cha Mkowela wilayani Tunduru,Mwakilishi wa Meneja wa RUWASA Wilaya ya Tunduru Emanuel Mfyoyi amesema mradi huo hadi kukamilika umegharimu zaidi ya shilingi milioni 163.

Amesema mradi huo umekamilika ukiwa na vituo vya umma saba vya kuchotea maji na vituo binafsi vinne na kwamba mradi huo una uwezo wa kuwahudumia  wananchi 1,720 waliopo katika kijiji cha Mloweka.

Akitoa taarifa ya mradi wa ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Muhwesi wilayani Tunduru kwa Kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru,Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tunduru Beatrice Mahengu,amesema mradi huo ambao haujakamilika hadi sasa  umegharimu shilingi milioni 80.

Amelitaja lengo kuu la mradi huo ni kuboresha huduma za afya kwa wananchi hasa mama na mtoto kwa kuwa

 majengo ya zahanati iliyopo sasa ni machakavu hivyo yanaathiri huduma za afya.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari wilaya ya Tunduru  Patrick Haule akitoa taarifa ya ukarabati wa majengo ya Tunduru sekondari kwa kiongozi wa mbio maalum za Mwenge wa Uhuru,amesema serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 792 kwa ajili ya ukarabati wa majengo ya shule hiyo.

Amesema mradi huo umekamilika na hivyo kuboresha mazingira ya kujifunzia  na kufundishia kwa walimu na wanafunzi na kuboresha afya za wanafunzi baada ya kurekebisha mfumo wa maji safi na maji taka.

Miradi mingine ambayo imepitishwa na mwenge wa uhuru wilayani Tunduru ni mradi wa ugawaji wa vyandarua kwa akinamama wajawazito na watoto ambao umegharimu zaidi ya shilingi milioni 94na mradi wa vifaa vya mahitaji maalum kwa wanafunzi wenye ulemavu ya zaidi ya shilingi milioni nne.

Miradi mingine ni mradi wa TEHAMA katika chuo cha Maendeleo ya wananchi Nandembo uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 100 na mradi wa ufugaji nyuki Nandembo wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 10.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba 2,2021

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.