• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru wakagua miradi nane Mbinga Mji

Imewekwa kuanzia tarehe: June 14th, 2024

MWENGE wa Uhuru umeendelea na mbio zake mkoani Ruvuma kwa kupitia miradi nane yenye thamani ya shilingi bilioni 2.1 katika Halmashauri ya Mji Mbinga.

Mwenge wa Uhuru ukiwa mjini Mbinga umekagua mradi wa ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje,jengo la maabara na jengo la upasuaji katika hospitali ya Halmashauri ya Mbinga,mradi ambao unatekelezwa kwa gharama ya Zaidi ya shilingi milioni 900.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo amesema mradi huo ukikamilika  utaongeza miundombonu toshelezi kwa watoa huduma na wagonjwa,kupanua wigo kwa watoa huduma za afya kwa makundi maalum na kuanzishwa huduma mpya za kuchunguzi.

Hata hivyo licha ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi huo,Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024 Godfrey Mnzava ameiagiza TAKUKURU  kufanya uchunguzi wa kina kwenye mradi huo,baada ya mwenge wa Uhuru kubaini utekelezaji wa mradi huo haukufanyika kupitia mfumo wa manunuzi ya umma wa NeST kama ilivyoelekezwa na serikali.

Mwenge wa Uhuru ukiwa mjini Mbinga umekagua mradi wa  kuboresha huduma ya maji safi katika Kijiji cha Utiri na kuweka jiwe la msingi,mradi ambao unagharimu  Zaidi ya shilingi milioni 421.

Mradi wa uboreshaji huduma ya maji safi Utiri unahudumia wakazi wapatao 3,857 ambapo lengo la mradi ni kusogeza huduma ya maji ili kuwapunguzia wananchi kero ya kutembea kutafuta maji.

Mradi mwingine ambao umefunguliwa na Mwenge wa Uhuru mjini Mbinga ni ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Myangayanga ambao umegharimu shilingi milioni 48.

Mwenge wa uhuru umeweka jiwe la kutembelea kiwanda cha kukoboa kahawa Mbinga ,mradi ambao umegharimu Zaidi ya shilingi milioni 725.

Akizungumza kwenye kiwanda hicho,Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Godfrey Mnzava amesema licha ya kiwanda hicho kuwa na manufaa kiuchumi ikiwemo kutoa ajira za kudumu 76 na za muda 300,ameuagiza uongozi kuwanunulia vifaa vya usalama kazini wafanyakazi wote wa kiwanda hicho.

Mwenge wa Uhuru mjini Mbinga umekagua mradi wa shamba la mbegu bora za miti  katika Kijiji cha Utiri lenye ukubwa wa ekari 23.8 linalomilikiwa na Halmashauri ya Mji wa Mbinga na kuendeshwa kwa ubia kati ya Halmashauri ya Wakala wa Misitu Tanzania (TFS)  kwa ufadhili wa Ubalozi wa Finland.

Mradi huo umegharimu Zaidi ya shilingi milioni 55 na kwamba lengo la mradi ni kuzalisha mbegu bora za miti ambazo zinapatikana kwa urahisi na kwa gharama nafuu.

Mwenge wa Uhuru ukiwa mjini Mbinga pia umepokea taarifa ya mapambano dhidi ya malaria ambapo Halmashauri imenunua vyandarua 43,955 vyenye thamani ya Zaidi ya shilingi milioni 404  ambavyo vimegawiwa bure kwa wajawazito, ,Watoto na wanafunzi ili kufikia adhima ya serikali ya Ziro Malaria ifikapo mwaka 2023.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.