• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE WA UHURU waridhia kuweka mawe ya msingi miradi mitano Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: April 19th, 2023

TAKUKURU waagizwa kuchunguza mradi wa sekondari ya Kawawa

MWENGE wa Uhuru 2023 umeridhia kuweka mawe ya msingi katika miradi mitano yenye thamani ya shilingi bilioni 1.6 katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Chiriku Chilumba anautaja mradi wa kwanza kuwa ni wa ujenzi wa kliniki ya afya ya kinywa na meno katika hospitali ya wilaya ya Namtumbo ambao serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 320 kutekeleza mradi huo ambao unatarajia kukamilika Aprili 30 mwaka huu.

Mradi mwingine ambao Mwenge wa Uhuru umeridhia kuweka jiwe la msingi ni ujenzi wa daraja la Libango ambao hadi sasa serikali imetekeleza mradi huo katika awamu mbili kwa kutoa zaidi ya shilingi milioni 900.

Hata hivyo amesema katika utekelezaji wa awamu ya tatu,serikali inatarajia kutoa shilingi milioni 300 katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 ili kukamilisha mradi huo ambao utakuwa umetumia shilingi bilioni 1.2

Mwenge wa Uhuru pia umeridhia kuweka jiwe la msingi katika mradi binafsi wa mgahawa na kiwanda kidogo unatekelezwa  mjini Namtumbo ambao unatarajia kugharimu shilingi milioni 120 ambapo hadi sasa kulingana na taarifa ya mmiliki wa mradi huo Romana Komba zimetumika shilingi milioni 80.

Komba amesema mradi huo unatarajia kutoa ajira za moja kwa moja kwa watu 20 na kwamba kiwanda kitakuwa na uwezo wa kutengeneza Mikate 1000 kwa siku na mgahawa una uwezo wa kutoa huduma kwa watu kati ya 50 hadi 100.

Mradi mwingine ambao Mwenge wa Uhuru umeridhia kuweka jiwe la msingi ni mradi wa ujenzi wa madarasa matatu katika shule ya sekondari ya Kawawa unaotekelezwa katika Kijiji cha Suluti ambapo serikali imetoa shilingi milioni 60 kutekeleza mradi huo.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023 Ndugu Abdalah Shaib Kaim amesema madarasa  matatu yamejengwa katika ubora.

Hata hivyo amesema kuna dosari kubwa kwenye nyaraka za manunuzi ya vifaa ambazo zimebainika hazipo na kwamba meza na viti 115 zilizopo kwenye madarasa hayo ni mbovu na hazikuzingatia ubora unaotakiwa.

Kutokana na hali hiyo amemuagiza Mkuu wa TAKUKURU wilayani Namtumbo kufanya uchunguzi   wa nyaraka za manunuzi na nyaraka za utoaji wa vifaa kutoka kwenye stoo.

“Afisa wa TAKUKURU ukibaini kuna upotevu wowote wa fedha za umma katika utekelezaji wa mradi huu sheria ichukue mkondo wake kwa mtu yeyote aliyehusika na upotevu huu’’,alisisitiza Shaib.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Aprili 18,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.