• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru watembelea miradi 11 ya bilioni 4.1 Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: June 9th, 2024

Mwenge wa Uhuru umetembelea miradi 11 yenye thamani ya shilingi bilioni 4.1 katika Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Peres Magiri  amesema Mwenge huo umekimbizwa  umbali wa kilometa 284 na kwamba ukiwa kwenye mkesha wilayani humo wananchi walijitokeza kupima afya zao.

Amesema jumla ya watu 173 walijitokeza kupima Virusi vya UKIMWI(VVU)  na hakuna hata mtu  mmoja aliyepatikana na maambukizi ya VVU na wananchi pia walijitokeza kuchangia damu kwa hiari.

Moja ya miradi iliyozinduliwa na Mwenge wa Uhuru wilayani Tunduru ni mradi wa ujenzi wa jengo la kutolea huduma za dharura (EMD) katika hospitali ya wilaya ya Tunduru ambapo serikali imetoa jumla ya shilingi milioni 369 kutekeleza mradi huo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo amesema mradi huo umekamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi ambapo hadi sasa jumla ya wateja 1,003 wamepatiwa huduma kupitia mradi huo.

Mradi mwingine ambao umepitiwa na Mwenge wa Uhuru wilayani Tunduru ni ujenzi wa mradi wa maji safi katika Kijiji cha Tuwemacho ambapo serikali imetoa Zaidi ya shilingi bilioni moja kutekeleza mradi huo.

Meneja wa RUWASA wilayani Tunduru Mhandisi Maua Mgallah  amesema mradi huo ukikamilika  utawanufaisha wananchi wapatao 3,527 hivyo kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama.

Akizungumza baada ya kukagua mradi wa maji,Kiongozi wa Mbio za Mwenge  wa Uhuru Kitaifa Godfrey Mnzava  ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo wa maji   ambao amesema utapunguza changamoto ya wananchi kutembea umbali mrefu kufuata maji.

Miradi mingine iliyotembelewa na Mwenge wa Uhuru wilayani Tunduru ni mradi wa ugawaji wa vyandarua kwa akinamama wajawazito na Watoto ambao umewezesha  wagonjwa wa malaria kupungua kutoka 99,469 mwaka 2021/2022 hadi wagonjwa 88,730 mwaka 2022/2023.

Mwenge wa Uhuru pia umetembelea mradi wa lishe,mradi wa ugawaji vifaa kwa makundi yenye mahitaji maalum na mradi wa ujenzi wa nyumba ya walimu ya familia mbili katika sekondari ya Kungu iliyojengwa kwa gharama ya shilingi milioni 95.

Mradi mwingine ni wa kituo cha  malezi ya vijana cha kilimo na mifugo la Kanisa la Upendo wa Kristo KIUMA ambapo mradi huo umegharimu Zaidi ya shilingi bilioni1.5,gharama zinazohusisha majengo, vitalu,nyumba,visima vya maji ya kumwagilia na mashine zake,bustani na mifugo

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.