• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAIBU Katibu Mkuu TAMISEMI avitaja vipaumbele vyake vitatu kufuta hoja za ukaguzi

Imewekwa kuanzia tarehe: November 14th, 2022


NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulika Menejimenti ya Tawala za Mikoa na Serikali  za Mitaa Ramadhan Kailima amevitaja vipaumbele vyake vitatu vya kufuta hoja za ukaguzi.

Kailima amevitaja vipaumbele hivyo wakati anazungumza kwenye kikao kazi  cha mawasilisho ya taarifa ya utekelezaji wa hoja za ukaguzi na maagizo yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali za mitaa(LAAC).

Kikao kazi hicho kilichowashirikisha wakurugenzi wa Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma,wakuu wa Idara na Menejimenti ya Mkoa kimefanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea Novemba 14 mwaka huu.

“Kipaumbele changu cha kwanza ni kufuta hoja  za ukaguzi,kipaumbele changu cha pili ni kufuta hoja za ukaguzi na kipaumbele changu cha tatu ni kufuta hoja za ukaguzi,vipaumbele vyangu vyote vitatu ni kufuta hoja za ukaguzi’’,alisisitiza Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI.

Kailima amezitaja hoja za ukaguzi zikifutwa ujenzi wa miradi mbalimbali kama vile vyumba vya madarasa,barabara na vituo vya afya na miradi mingine,utafanyika kwa viwango na thamani ya fedha itaonekana.

“Sitakuwa na msamaha kwa mtendaji yeyote ambaye atakuwa anazalisha hoja kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake,ukizalisha hoja usitarajie kuhamishwa,biashara yako itaishia hapo hapo,utaondolewa kwenye nafasi uliopo’’,alisisitiza Naibu Katibu Mkuu.

Kulingana na Naibu Katibu Mkuu huyo,ukifuta hoja ya ukaguzi wa fedha kwenye benki,itasababisha fedha kupelekwa benki na mapato ya Halmashauri husika yataongezeka.

Ameongeza kuwa ukifuta hoja ya watumishi ambao hawajalipwa fedha zao za likizo,ni kwamba watumishi hao watalipwa fedha zao za likizo kwa wakati na kuboresha utendaji wao wa kazi.

Kwa mujibu wa Kailima,ukifuta hoja za malimbikizo ya watumishi na stahili zao mbalimbali,itawezesha watumishi hao kupata stahili zao kwa wakati na kupunguza manung’uniko kwa watumishi na kuongeza ufanisi wa kazi.

Hata hivyo amesema ukifuta hoja ya kununua bidhaa ambazo hazijapokelewa ina maana kuwa bidhaa hizo zitapolewa na kufuata taratibu za manunuzi hivyo hoja hazitakuwepo.

Amesisitiza kuwa hoja za ukaguzi zikifutwa zitawezesha viongozi wa kitaifa wakiwemo wabunge watakuwa wanaangalia thamani ya miradi iliyotekelezwa.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Stephen Ndaki akizungumza kwenye kikao kazi hicho amewaasa wakuu wa Idara kujibu hoja za ukaguzi  kwa timu na  kila mmoja kuwajibikaji kikamilifu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Novemba 14,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.