• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAIBU Waziri wa maji akagua miradi ya mabilioni Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: April 11th, 2021

Naibu Waziri wa Maji MaryPrisca Mahundi amefanya ziara ya kikazi Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma kwa kukagua miradi ya maji ya mabilioni ya fedha.

Katika ziara hiyo Mahundi amekagua mradi wa maji wa Kipapa na Mhilo ambao umetekelezwa kwenye Kata za Kipapa na Langiro, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wenye thamani ya shilingi Milioni 647.4

Mradi huo umekamilika na umeanza kuhudumia wananchi kwa kutoa maji safi na salama.

Naibu Waziri wa Maji  pia ametembelea na kukagua miradi mingine miwili ya maji ambayo ni mradi katika Kijiji cha Lifakara unaokadiriwa kugharimu Shilingi Milioni 651 na mradi unaojengwa Kata ya Bethlehemu ambao unatarajia  kugharimu  sh.Bilioni 1.4 hadi kukamilika kwake.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa maji pia amekagua miradi ya maji inayotekelezwa kwenye vijiji vya Amani Makolo, Mabuni, Luhagara na Litumbandyosi wilayani Mbinga.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo Naibu Waziri wa Maji ametoa mwezi mmoja kwa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Ruvuma(RUWASA) kuongeza vituo vya kuchotea maji kwenye kitongoji cha Kiosi, Kijiji cha Kipapa.

“RUWASA hakikisheni mnaanza utekelezaji wa mradi wa kusambaza maji kwenye Kijiji cha Langiro Asili, Kata ya Langiro ndani ya kipindi cha miezi mitatu ijayo’’,alisisitiza Mahundi.

Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshongwa ametoa rai kwa wananchi kutunza vyanzo vya maji sanjari  na miundominu ya maji iliyopo kwenye maeneo yao ili miradi hiyo iweze kudumu kwa muda mrefu na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Aprili 12,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.