• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAIBU Waziri wa Maji aweka jiwe la msingi mradi wa maji Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: December 18th, 2024

WATANZANIA  wametakiwa kuwa na tabia ya kushirikiana na Serikali na kuiunga mkono katika ujenzi wa miradi  mbalimbali ya maendeleo ikiwemo  miradi ya maji  yenye mchango mkubwa katika kuchochea na kuharakisha maendeleo yao.


Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew ,wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vya Misechela na Liwanga baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa mradi mkubwa wa maji unaotekelezwa na Serikali kwa gharama ya Sh.bilioni 3.02.


“Mambo makubwa  yanayofanywa na Rais wetu Samia Suluhu Hassan,Mbunge wetu Idd Mpakate na Diwani wetu ni nzuri sana,kwa hiyo  lazima tuwatie moyo na tuwaunge mkono,ili waendelee kufanya mambo makubwa zaidi”alisema Kundo.


Kundo alisema,Serikali ya awamu ya sita  chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inawajali Watanzania ndiyo maana inawaletea na kutekeleza miradi mingi ya maendeleo  wilayani Tunduru na maeneo mengine hapa nchini ambayo imetoa fursa kwa wananchi kujikita kwenye shughuli zao za kiuchumi.


Alisema,kwa muda mkoa wa Ruvuma hususani wilaya ya Tunduru haikuwa na huduma ya maji ya uhakika,lakini katika kipindi kifupi Serikali sikivu ya Rais Samia Suluhu Hassan imeleta miradi zaidi ya 32 ya maji katika mkoa huo ikiwemo mradi wa maji Misechela.


Alisema,mradi wa Misechela utakapokamilika utamaliza kabisa changamoto ya huduma ya maji safi na salama na amewahakikishia wananchi  kwamba mradi huo utakamilika kama Serikali ilivyopanga.


“Pia katika kupunguza changamoto ya maji katika jimbo la Tunduru kusini, Serikali ya Chama cha Mapinduzi imechimba visima vya maji katika vijiji  mbalimbali ikiwemo kijiji cha Mdingula na Azimio na kutekeleza miradi ya maji katika vijiji mbalimbali”alisema Kundo.


Kundo alisema,Rais Samia Suluhu Hassan ameonyesha mapenzi makubwa kwa wananchi wa Misechela kwa kutoa fedha nyingi ambazo zitatumika kutekeleza mradi huo ili kuwaondolea  kero ya kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta huduma ya maji.


Meneja wa Ruwasa wilaya ya Tunduru Maua Mgallah alisema,mradi wa maji Misechela-Liwanga unaotekelezwa katika Halmashauri ya wilaya Tunduru unategemewa kusambaza maji katika vijiji viwili vya Liwanga na Misechela na unatekelezwa kwa fedha za Serikali kupiti program ya malipo kwa matokeo(Pfor4).


Mgallah ametaja kazi zilizopangwa kutekelezwa katika mradi huo ni ujenzi wa tenki la ujazo wa lita laki tatu,ujenzi wa tenki la chini lenye uwezo wa kuhifadhi lita elfu sabini na tano na kujenga banio.


Kwa mujibu wa Mgalalah kazinyingine zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na uchimbaji mitaro na kulaza bomba, kujenga vituo vya kuchotea maji,nyumba ya mitambo,kufunga umeme jua na ujenzi wa ofisi ya Jumuiya ya watumia maji ngazi y jamii(CBWSO).


Pia alisema,wilaya ya Tunduru ina jumla ya vijiji 139 vinavyohudumiwa na Ruwasa kati ya hivyo vijiji 119 vimefikiwa na huduma ya maji na upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi ni wastani wa asilimia 70.20 ambayo ni sawa na watu 236,138 kati ya watu 336,380.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.