• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NDOTO ya maji safi yatimia Ruvuma;Bilioni 228.92 zaleta mapinduzi makubwa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 30th, 2025

Miaka michache iliyopita, maji safi yalikuwa ndoto kwa familia nyingi mkoani Ruvuma. Kina mama walitembea kilometa nyingi kila alfajiri na watoto walikosa masomo wakisaka tone la maji. Lakini leo, hali hiyo imegeuka kuwa simulizi ya zamani. 

Kwa uwekezaji wa zaidi ya shilingi bilioni 228.92, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  kupitia miradi mbalimbali imeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya maji—kutoka vijijini hadi mijini, kila kona ya Ruvuma sasa inanufaika na huduma bora za maji safi na salama.

Katika halmashauri zote nane za mkoa  wa Ruvuma miradi ya maji imetekelezwa kwa kasi na ubora wa hali ya juu. Kupitia juhudi hizo, wananchi wanafurahia upanuzi wa mtandao wa maji safi uliowafikia maelfu ya wakazi waliokuwa wakikosa huduma hiyo ya msingi kwa miaka mingi. Mitandao mipya ya mabomba, matenki ya kisasa na visima virefu vimejengwa, huku huduma zikifikishwa hadi kwenye taasisi za umma kama shule, vituo vya afya na maeneo ya biashara.

Mji wa Songea, ambao ni kitovu cha maendeleo ya mkoa, umeshuhudia utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji  unaogharimu shilingi bilioni 145 unaotegemewa kuwa mkombozi wa kudumu kwa wakazi wake. Mradi huu umejumuisha ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya uchujaji na usambazaji wa maji, hatua ambayo imerahisisha upatikanaji wa maji kwa zaidi ya asilimia 90 ya wakazi. A

Sauti za shukrani kutoka kwa wakazi wa  Mkoa wa Ruvuma sasa zinasikika kila kona,kutoka kwa wakulima waliopata muda zaidi wa kushughulikia mashamba yao, hadi kwa wanafunzi waliopata fursa ya kuhudhuria masomo bila bughudha ya kutafuta maji. 

Hakika, uwekezaji huu si tu umeleta maji, bali umeleta hadhi, afya na matumaini mapya kwa wakazi wa Ruvuma. Ni ushahidi kuwa pale dhamira ya kweli inapowekwa, maendeleo halisi yanawezekana na maji siyo tu uhai, bali ni kichocheo cha mapinduzi ya kijamii na kiuchumi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.