• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NEMC yatoa siku 30 kwa wamiliki wa migodi Ruvuma kusajili miradi

Imewekwa kuanzia tarehe: December 13th, 2024

Baraza la Taifa la Hifadhi na usimamizi wa Mazingira NEMC limetoa siku 30 kwa wamiliki, waendeshaji wa Migodi na vituo vya kuuzia na kuhifadhia Makaa ya mawe kuhakikisha wanasajili miradi yao  ili  kupata vyeti vya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) na kuhakiki ndani ya siku 30 kuanzia Disemba 8, 2024.

Wito huo umetolewa kufuatia ukaguzi uliofanyika katika vitalu mbalimbali vya migodi na kubaini makosa yanayokiuka Sheria ya usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za Mkoa wa Ruvuma mara baada ya zoezi la ukaguzi huo, Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria wa NEMC, Bw. Jamal Baruti ameorodhesha makosa yaliyobainishwa katika ukaguzi huo yakiwemo; Kutofanyika kwa Tathmini ya Athari za Mazingira (TAM), ukosefu wa mifumo ya usimamizi wa Mazingira, kutelekezwa kwa migodi pasipo kukarabati Mazingira, Uchafuzi wa vyanzo vya maji na hewa, kuongeza mawanda ya shughuli za migodi bila taarifa na idhini ya kisheria, kukosekana kwa taarifa za Upelembaji za kila mwaka na kukosekana kwa Mipango ya urejeshaji Mazingira.

Ukaguzi huo uliofanywa na timu ya wataalam kutoka NEMC kwa kushirikishana na wamiliki wa migodi umefanyika katika migodi 16 kati ya 18, maeneo ya biashara za makaa ya mawe 7 kati ya 15 na maeneo 2 ya utafiti kuanzia Novemba 27 hadi Desemba 8, 2024 katika Wilaya za Madaba, Songea, Nyasa na Mbinga Mkoani Ruvuma.

Sambamba na hayo, timu hiyo ya ukaguzi imetoa elimu elekezi kwa wamiliki wa migodi ikiwemo kuweka miundombinu ya kudhibiti uchafuzi wa Mazingira, na  ukarabati endelevu wa Mazingira,

Aidha Bw. Baruti amesisitiza kuwa Baraza litaendelea kutoa maelekezo na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara Kwa wamiliki wa migodi ili kuhakikisha uzingatiaji wa Sheria na utekelezaji maagizo yaliyotolewa na kuto sita kuchukua hatua za kisheria kwa wadau wote watakaoshindwa kutekeleza maelekezo haya ikiwa ni pamoja na kupewa adhabu au kusimamisha shughuli zao ili kulinda Mazingira, afya ya jamii na kuhakikisha uwiano wa maendeleo ya kiuchumi, uhifadhi wa Mazingira  na rasilimali za Taifa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.