• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NFRA kuanza kununua mahindi ya Ruvuma Agosti 15 mwaka huu

Imewekwa kuanzia tarehe: August 8th, 2021

SERIKALI imetangaza rasmi kuanza kununua mahindi kupitia wakala wa hifadhi ya Taifa(NFRA) Mei 15 kwa bei ya Sh 500 katika mikoa yote inayolima zao hilo,ikiwemo kwenye kituo cha NFRA Kanda ya Songea

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa  na Naibu Waziri wa kilimo Hussen Bashe, wakati akiongea na viongozi wadau wa kilimo na viongozi wa ngazi mbalimbali wa wilaya ya Tunduru katika kikao cha kazi ambacho pia kilihudhuriwa na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigadia Jenerali Wilbert Ibuge.

Waziri Bashe amesema,Serikali imeamua kununua kwa bei ya 500 kutokana na wafanyabiashara kununua mahindi kwa Sh 250 ambayo hailingani na halisi ya uzalishaji, na hatua hiyo  itasaidia sana kuwalinda wakulima ili kuwahi maandalizi ya msimu mpya wa kilimo 2021/2022.

Aidha, amewapongeza viongozi wa serikali ya wilaya ya Tunduru wakiongozwa na Mkuu wa wilaya Julius Mtatiro kwa kazi nzuri wanayofanya kusimamia suala la kilimo hususani kilimo cha zao maarufu la korosho ambalo ndilo  linaloongoza kuipatia Serikali mapato  makubwa ya fedha kigeni hapa nchini.

Amesema, lengo la wizara ya kilimo ni uzalishaji wa zao la korosho ni kuzalisha tani laki saba kwa mwaka,hata hivyo uzalishaji  wa zao hilo unaendelea kuanguka kitakwimu ambapo katika wilaya hiyo inayosifika kwa uzalishaji  hapa nchini unaendelea kushuka mwaka hadi mwaka.

Kwa mujibu wa Waziri Bashe,katika wilaya ya Tunduru uzalishaji umekuwa wa kusua sua kwani takwimu zinaonesha kuwa mwaka 2016/2017 uzalishaji ulikuwa tani 15,310 mwaka 2017/2018 uzalishaji ulikuwa tani  20,000 mwaka 2018/2019  tani elfu 18, na mwaka 2020/2021 uzalishaji wa zao hilo ulishuka zaidi hadi kufikiwa tani elfu 14.

Amesema,ni lazima wadau wa kilimo wakiwemo wakulima wajiulize tatizo la kuongezeka kushuka kwa uzalishaji huo katika wilaya ya TunduruKwa mujibu wa Waziri Bashe,tatizo kubwa la kushuka kwa uzalishaji wa zao hilo linatokana na watu  waliopewa dhamana hasa wataalam wa kilimo kushindwa kuwafuatilia  na kuwasimamia wakulima kwa kwa wakati kuwapa elimu ya kilimo bora jambo linalosababisha wakulima kuendelea na kilimo cha mazoea.

Hivyo amesema, Serikali ina wajibu kuhakikisha inawafuatilia wakulima kujua changamoto wanazokabiliana nazo na kuwapa elimu ya kilimo bora na chenye tija, badala ya kuwaacha wakiangaika na kuendelea kulima kwa mazoea.

Pia amesema, Serikali kupitia wizara ya kilimo imetafakari na kuamua kumuondolea  mkulima mzigo wa pembejeo kwa kutoa pembejeo za ruzuku  bure na mkazo mkubwa ni kupeleka dawa za maji badala ya dawa za unga na zitafikishwa kwa kila chama cha msingi cha Ushirika.

Amesema, matarajio katika wilaya hiyo ni kupata dawa za maji lita 130,000  na tayari lita 48,000,dawa aina ya Salphur kilo milioni 2.7 na ambazo zimeshafikishwa katika wilaya hiyo ni zaidi ya  lita laki 9  ambapo wizara ya kilimo itahakikisha dawa zilizobaki zitawafikia wakulima.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma  Brigadia Jenerali Wilbert Ibuge amemueleza Naibu Waziri kuwa, katika wilaya hiyo asilimia 85 ya ardhi yake inafaa kwa kilimo hata hivyo ni asilimia 15 tu ndiyo inayotumika kwa ajili ya shughuli za kilimo.

Amesema, katika mkoa wa Ruvuma yenye watu takribani milioni 1.6 uzalishaji wa chakula kwa mwaka  2019/2020 ulikuwa tani 787.321 wakati mahitaji ilikuwa tani 469,172 hivyo kuwa na ziada ya chakula tani 318,149,mwaka 2021 uzalishaji ulikuwa tani 816,242 na hivyo kuwa na ziada ya tani 345,000.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro amesema,wilaya ya Tunduru imekuwa ikifanya vizuri katika uzalishaji wa mazao mbalimbali,hata hivyo wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo Tembo wanaovamia mashamba na kuharibu mazao  na  ufugaji holela wa mifugo na kama changamoto hizo isipopatiwa majibu kwa haraka hali ya uzalishaji katika wilaya hiyo utashuka kwa kiwango kikubwa.

Mtatiro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama amesema,  changamoto nyingine ni kuwepo kwa Viuatilifu feki vinavyoingizwa sokoni na kuwauzia wakulima jambo linalokwamisha sana juhudi kubwa zinazofanywa na wakulima.

Amesema, katika wilaya hiyo asilimia 83 ya ardhi yake inafaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali,hata hivyo bado wakulima wanahitaji maelekezo na msukumo wa wataalam ili wakulima waweze kuzalisha kwa tija.

Imeandikwa na Muhidin Amri,Tunduru.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.