• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NMB yaipiga jeki hospitali ya Wilaya Namtumbo vifaa vya milioni kumi

Imewekwa kuanzia tarehe: March 10th, 2021

Benki ya NMB  imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya hospitali ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma vyenye thamani ya shilingi milioni kumi.

Akikabidhi vifaa katika hafla iliyofanyika katika hospitali hiyo mjini Namtumbo,Meneja wa NMB Kanda ya Kusini Janeth Shango amevitaja vifaa hivyo kuwa ni vitanda vitano vya wagonjwa na godoro zake.

Vifaa vingine amevitaja kuwa ni vitanda viwili vya kisasa vitakavyotumika wakati wa kujifungua akinamama na mashuka 25 kwa ajili ya vitanda hivyo.

“Kwa miaka kadhaa sasa NMB imekuwa ikisaidia miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi kwa kujikita zaidi kwenye miradi ya elimu kwa kutoa madawati na vifaa vya kuezekea na kwenye afya kwa kutoa vitanda na magodoro yake’’,alisema.

Amesisitiza kuwa kupitia jamii,NMB inatambua kuwa wanapatikana wateja wake wengi,kwa hiyo kurudisha sehemu ya faida kwa jamii ni utamaduni wa Benki hiyo ambayo imezifikia wilaya zote nchini kwa asilimia 100.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo ,Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo ameishukuru Benki ya NMB kwa msaada huo ambao amesema umeongeza vitanda  katika hospitali hiyo ambayo imeanza kulaza wagonjwa na kwamba kabla ya msaada huo ilikuwa na vitanda kumi tu.

“Tuliamua kuanzia mwaka jana kuanza kulaza wagonjwa,hivyo tulianza na vitanda kumi,leo NMB wametuletea vifaa vya milioni kumi kwa ajili ya kusaidia hospitali yetu,tunawashukuru sana’’,alisisitiza Kizigo.

Hata hivyo amesema NMB katika wilaya ya Namtumbo  imekuwa karibu na shule kwa kutoa madawati na vifaa vya ujenzi na imetoa mikopo kwa ajili ya wakulima wa tumbaku.

Mary Ponera Mkazi wa Namtumbo ameishukuru NMB kwa msaada wa vitanda ambavyo amesema ni muhimu kwa wajawazito wakati  wanafika kujifungua katika hospitali hiyo.

Benki ya NMB katika nchi nzima ina matawi 225,mashine za kutolea fedha ATM zaidi ya 800,wakala zaidi ya 6,000 na idadi ya wateja zaidi ya milioni tatu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 10,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • MWENGE wa uhuru waingia Pers

    May 10, 2025
  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.