• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NMB yazindua tisheti 500 zitakazotumika katika tamasha la Majimaji Selebuka

Imewekwa kuanzia tarehe: August 11th, 2020

Benki  ya NMB Tawi la Songea  mkoani Ruvuma imezindua rasmi tisheti 500 zilizogharimu shilingi milioni tano kwa ajili ya Tamasha la Majimaji Selebuka spesho.

Tisheti hizo  zitatumika kwa wanafunzi watakaoshiriki  midaharo itakayofanyika kwenye tamasha hilo  la Majimaji Selebuka ambalo litafanyika kwa siku saba katika uwanja wa Majimaji mjini Songea .

Akizungumzia Tamasha hilo Meneja wa NMB kanda ya kusini Janeth Shango amesema Tamasha hilo  limelenga kuendeleza Utalii wa Mkoa wa Ruvumu,ujasiriamali  na kukuza Michezo kwa wanafunzi  na kwa watu wazima.

‘’ NMB tukiwa jirani ya jamii na kama  wadau wa wajasiriamali, tumeona ni vema kushiriki katika tamasha hili ili tuweze kushirikiana na kusaidia  kufanya tamasha hili liweze kuwa zuri zaidi mwaka huu’’,alisisitiza.

Shango amesema Benki ya NMB watakuwepo katika viwanja vya majimaji kwa wiki moja na watatoa huduma za kifedha  na kutoa Elimu kwa wajasiriamali, na wanafunzi  watafundishwa jinsi ya kujiwekea akiba, pamoja na mambo yote  yanayohusiana na mikopo na ufunguzi wa akauntina namna ya kuendesha.

Hata hivyo Meneja wa NMB kanda ya kusini amesema watakuwa na wataalamu wa Kilimo na watatoa Elimu kwa wakulima jinsi gani wafanye wanapotaka kulima na kuvuna mazao kwa wingi.

Kwa upande wake Meneja wa NMB Tawi la Songea Daniel Zake amewashukuru wananchi kwa kuwa wateja wa Benki ya NMB ambapo katika tamasha hilo NMB watakuwa na masomo mbalimbali ya vikundi vidogovidogo,Benki jamii(VICOBA)  na jinsi ya kujiwekea akiba kwa Fedha ndogo walizonazo ili  kukuza kipato katika maisha yao.

‘’Tamasha  la Maji maji Selebuka ni tamasha kubwa ambalo linakuwa na mambo mengi ya kujifunza hasa katika elimu ya  Kifedha  kwa upande wa mikopo na riba nafuu na kutumia mifumo ya kidijitali na namna gani   unaweza kuwa nyumbani na kufanya miamala Mbalimbali na kuwahudumia waliombali kupitia simu ya mkononi’’,alisisitiza Zake.

Zake amesema Katika tamasha hilo itakuwa sehemu sahihi kupokea maoni kwa wateja wa NMB na  jinsi gani  wanaweze kufanya vizuri ka ili waweze kuhudumia wateja kwa kile wanachokitarajia wateja wa Mkoa wa Ruvuma kutoka Benki ya NMB.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari   wa  Mkoa wa Ruvuma

Agosti 11,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.