• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

OFISI ya Waziri Mkuu,FAO Yawapongeza maafisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: October 10th, 2020

MAAFISA wa Habari wa Mkoa wa Ruvuma wamepongezwa na Ofisi ya Waziri Mkuu  na Shirika la  Chakula na Kilimo  Duniani(FAO)  kwa kuwataarifa wananchi kwa kusahihi  mafunzo ya utayari wa kukabiliana na magonjwa ya mlipuko yaliofanyika kwa siku tano katika hoteli ya Tiffany Diamond mjini Mtwara.

Akizungumza wakati wa ufungaji mafunzo hayo ambayo yalishirikisha  timu za dharura za kukabili magonjwa kutoka mikoa hatarishi ya Ruvuma na Mtwara,Valentina Sanga wa Idara ya Maafa Dawati la Afya Moja Ofisi ya Waziri Mkuu,amesema wanahabari hao licha ya kushiriki katika mafunzo hayo pia wamekuwa wanatimiza kazi ya kuhabarisha umma kwa siku zote za mafunzo kupitia vyombo mbalimbali vya habari

Ametoa rai kwa wanahabari wengine nchini kuiga mfano wa wanahabari hao ambao pia katika mafunzo hayo katika mtihani wa mwisho wa kujipima wamefanya vizuri na kupewa vyeti vya kuhitimu mafunzo hayo.

Sanga amelishukuru Shirika la FAO kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu kufanikisha  mafunzo hayo  na kuwapongeza wakufunzi wote kutoka Chuo cha SUA,Wizara ya Afya na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kufanikisha mafunzo hayo ambayo yamesaidia kuelewa dhana ya afya moja ambayo itasaidia kupunguza gharama kwa kushirikiana.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Chakula na Kilimo Duniani Dr.Niwael Mtui amesema wanahabari hao wamefanya kazi iliyotukuka na kwamba wanastahili pongezi kwa sababu wamekuwa wanapigiwa simu kutoka sehemu mbalimbali kutokana na kusoma na kuangalia habari mbalimbali zilizochapishwa kwenye magazeti,redioni,luninga za mitandaoni  na kutangazwa kwenye mitandao  mbalimbali ya kihabari.

“Wanahabari ni miongoni mwa wadau wanaounda timu za dharura za kukabiliana na magonjwa ya mlipuko,wadau wengine ni wataalam wa afya,mifugo,mazingira,maliasili hivyo naomba mafunzo yote ambayo tumepata twende kushare na  wenzetu ambao hawajapata nafasi ya mafunzo’’,alisema.

Dr.Mtui amesisitiza kuendelea kushirikiana na kwamba ndani ya siku tano wadau wameweza kufahamiana jambo ambalo litakuwa rahisi kushirikiana  kwa kupeana taarifa za milipuko ya magonjwa sita ya kipaumbele Ili kuchukua hatua haraka.

Naye Mwakilishi wa washiriki  wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr.Jairy Khanga ameipongeza Ofisi na Waziri Mkuu na FAO kwa kutoa mafunzo ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko katika mikoa ya Ruvuma na Mtwara.

“Hii ndiyo mikoa pekee ambayo ilikuwa haijapata mafunzo hayo,mikoa hii ya kusini ambayo inapakana na nchi jirani ipo katika hatari ya kupata magonjwa ambukizi ya mlipuko hivyo mafunzo haya ni muhimu sana’’,a asisitiza Dr.Khanga.

Imeandikwa na maafisa Habari serikalini

Oktoba 20,2020

Mtwara

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.