• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ONGEZENI jitihada za kupambana na UKIMWI

Imewekwa kuanzia tarehe: November 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amesema jitihada na mapambano yanahitajika ili kupunguza kiwango cha maambukizi ya virusi vya UKIMWI katika mkoa huo.

Amesema hayo wakati akifanya uzinduzi rasmi wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo kitaifa itafanyika mkoani Ruvuma Disemba Mosi mwaka huu, ambapo uzinduzi huo umefanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma.

"Kiwango cha maambukizi katika mkoa ni 4.9% kiwango hiki kimepungua ambapo tulikuwa katika wastani wa 5.6% kwa mwaka 2017, bado kiwango hiki ni cha juu, tunahitajika kuendeleza jitihada na mapambano ili kuweza kukipunguza kwa kiwango kinachotakiwa au kinachoelekezwa," alisema Kanali Ahmed.

Ameongeza kuwa maambukizi mapya yanatokana na vichocheo mbalimbali, hivyo amesisitiza kuendelea kudhibiti vichocheo hivyo na kutoa Elimu katika shughuli za kiuchumi zinavyoongezeka ili kupambana dhidi ya janga hilo.

Kupitia kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ambayo ni "Chagua Njia Sahihi, Tokomeza UKIMWI," Kanali Ahmed amewasisitiza wananchi kuendelea kuchagua njia sahihi kwa ajili ya kutokomeza UKIMWI.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Jumanne Issango, amesema kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ya mwaka huu haiitaji ufafanuzi mkubwa kwa kuwa Elimu ya njia hizo zimekuwa zikitolewa katika majukwaa mbalimbali ili kuhimiza namna ya kutokomeza UKIMWI.

Ameongeza kuwa uchaguzi wa kauli mbiu hiyo ambao unaletwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la  Kudhibiti UKIMWI ni hatua muafaka ambayo ikizingatiwa  jamii itafika mahali pazuri.

Kwa upande wake mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Dr. Catherine Joachim ameupongeza uongozi wa mkoa wa Ruvuma na wananchi wake wote kwa kupiga hatua katika mapambano dhidi ya VVU kwa kuwa katika mkoa wa Ruvuma kiwango chake kimepungua toka 5.6% kwa mwaka 2016/17 hadi 4.9% mwaka 2022.

Ameongeza kuwa takwimu zinaonyesha kuwa mkoa wa Ruvuma unaoongoza kwa upimaji wa VVU ambapo utafiti wa mwaka 2023 umeonyesha kuwa 82% ya wananchi wa mkoa wa Ruvuma wanatambua hali zao za maambukizi na 97% ya watu wenye maambukizi wanatumia dawa za kufubaza  virusi vya UKIMWI.

Amesisitiza kuwa wao kama Wizara ya Afya inaukumbusha umma kuwa UKIMWI bado upo na ni janga la Taifa na bado unaendelea kusababisha vifo kwani hakuna chanjo wala tiba hivyo wananchi waendelee kuchagua njia sahihi ili kutokomeza UKIMWI.

Kiwango cha maambukizi ya virusi vya UKIMWI katika Mkoa wa Ruvuma kimeshuka kutoka 5.6% kwa mwaka 2016/17 hadi kufikia 4.9% mwaka 2022.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.