• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RAIS SAMIA aipongeza Benki ya Maendeleo Afrika kwa kuwekeza kwenye miundombinu Tanzania

Imewekwa kuanzia tarehe: September 26th, 2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameishukuru na kuipongeza Taasisi ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuwa mdau mkubwa wa sekta ya miundombinu nchini ambapo wamewezesha mkopo wa Shilingi Bilioni 630 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 66) kwa kiwango cha lami na barabara nyingine.

Dkt. Samia ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na wananchi Wilayani Nyasa mara baada ya kufungua barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 16) iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi Bilioni 122.76 Mkoani Ruvuma.

“Nataka niwaambie benki ya AfDB hawajasaidia barabara hii peke yake, ni wadau wetu wa barabara nchi nzima na hivi tunavyozungumza wanatusaidia kujenga barabara ya mzunguko ya njia nne katika mji Mkuu wa Dodoma”, Amekaririwa Dkt. Samia.

Dkt. Samia ameeleza kuwa kukamilika kwa barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 66) kwa kiwango cha lami utasaidia kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa abiria na bidhaa na amewataka wananchi kutumia uwepo wa barabara hiyo kuleta maendeleo katika Wilaya ya Nyasa na Mkoa wa Ruvuma kiujumla.

Aidha, Dkt. Samia ametoa wito kwa watumiaji wa barabara hiyo hususani madereva kuwa waangalifu ili barabara iweze kudumu kwa muda mrefu zaidi.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuendelea kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ambapo wamekamilisha kujenga kwa kiwango cha lami mtandao wa barabara zenye urefu wa kilometa 2,384 ambayo ni sawa na asilimia 20 ya mtandao wote wa barabara unaosimamiwa na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS).

Kadhalika, Bashungwa ameeleza kuwa Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS ipo katika hatua za kutafuta Wakandarasi kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni Daraja la Mkili lenye urefu wa mita 20 pamoja na Daraja la Mitomoni lenye urefu wa mita 80 ambalo litaunganisha Wilaya ya Nyasa na Songea Vijijini.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Patricia Laverley, ameleeza utekelezaji wa mradi huo ni sehemu ya urafiki kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki hiyo na kusema kuwa kukamilika kwa barabara ya Mbinga – Mbamba Bay kutasaidia kupunguza muda wa safari, nauli pamoja na gharama za matengenezo.

Awali akitoa taarifa ya mradi huo, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta ameeleza kuwa Barabara ya Mbinga – Mbamba Bay (km 66) imefadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika chini ya mradi wa “Transport Sector Support Programme” (TSSP) na kutekelezwa na Mkandarasi China Henan International Cooperation Group kutoka China na Mhandisi Mshauri kutoka SMEC International Pty kutoka Australia kwa gharama ya Shilingi Bilioni 122.76


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.