• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RAIS wa Ujerumani alivyowafariji wahanga wa vifo 67 vilivyotokea Songea miaka 117 iliyopita

Imewekwa kuanzia tarehe: November 1st, 2023

Na Albano Midelo,Songea

Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Dkt.Frank Walter Steinmeier amewafariji wahanga wa tukio la vifo vya mashujaa 67 waliua kikatili na wakoloni wa Kijerumani miaka 117 iliyopita mjini Songea mkoani Ruvuma.

Wakoloni wa kijerumani waliwauawa kikatili kwa kuwanyonga mashujaa wa vita ya Majimaji wapatao 67 wakiongozwa na Jemedari wa kabila ya wangoni Nduna Songea Mbano mwaka 1906 kisha kuwazika katika makaburi mawili ndani ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea.

Akizungumza baada ya kutembelea Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea na kuzungumza na wahanga wa tukio hilo,Rais wa Ujerumani Dkt.Steinmeier amesema baada ya matukio ya vifo vya watu 67 yaliyotokea hapa Songea  miaka 117 iliyopita,yeye kama Rais wa Ujerumani amepata fursa ya kukutana na wahanga kwenye eneo la tukio na kuwaomba msamaha kwa kilichotokea.

Amesema ameguswa na historia ya shujaa wa wangoni Nduna Songea Mbano na mashujaa wengine 66 ambao amesema historia yao ni ya kuhuzunisha sana hasa vifo vyao ambavyo waliuawa kikatili kwa kunyongwa.

“Leo baada ya kufika hapa Songea nimefahamu kuhusu jambo la kinyama walilotendewa mashujaa hawa limeendelea kuathiri familia nyingi hadi leo,ni watu wachache sana wanaofahamu historia hii nchini Ujerumani’’,alisisitiza Rais wa Ujerumani.

Amesema Mji wa Songea unawakilisha upinzani wa watanzania dhidi ya ukoloni wa kijerumani na kuongeza kuwa amefika Songea ili kubeba historia hiyo na kuipeleka kwa wajerumani wengi atakaporejea nchini kwake.

Hata hivyo amesema matukio yaliyotokea Songea miaka 117 iliyopita ni matukio yanayohusu jamii za nchi mbili za Tanzania na Ujerumani ambapo amesisitiza kuwa nchi ya Ujerumani lazima iwajibike kuhusu historia ya vita ya Majimaji ili kujenga kwa Pamoja Maisha ya siku za usoni.

Amemtaja Jemadari wa wangoni Songea Mbano kuwa alikuwa kiongozi shupavu katika vita ya Majimaji dhidi ya ukoloni wa kijerumani waliotawala kwa ukatili mkubwa.

Amesema baada ya kuzungumza na familia ya Songea Mbano ameguswa na mambo yote aliyoelezwa,waliyoyafanya majeshi ya wakoloni wa kijerumani.

“Mimi kama Rais wa Ujerumani naomba msamaha kwa mambo yote ambayo wajerumani waliwatendea  mabibi na mababu zenu miaka 117 iliyopita,nawahakikishia kwamba sisi wajerumani tutajitahidi kupata majibu ya maswali yote ambayo hayana majibu na ambayo hayawapi amani’’,alisisitiza Dkt. Steinmeier.

Akizungumzia kuhusu masalia ya watu waliouawa miaka 117 iliyopita Rais huyo amesema masalia hayo kutoka Afrika Mashariki yalisafirishwa hadi nchini Ujerumani na kuhifadhiwa katika makumbusho na hifadhi za kiatropolojia ambako kuna maelfu ya mafuvu ya vichwa vya binadamu.

Amesema serikali ya Ujerumani inaendelea na jitihada za kutafuta fuvu la kichwa cha shujaa Songea Mbanonchini Ujerumani ambapo ameitaja changamoto kubwailiyopo ni kupima na kutambua  masalia halisi ya binadamu kwa fuvu la mlengwa.

Hata  hivyo amesema Tanzania na Ujerumani ni nchi ambazo zinaunganishwa na mambo mengi ikiwemo miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.

Ameongeza kuwa Tanzania na Ujerumani pia zimeunganishwa na historia  ya mashujaa wa Majimajiambapo amesema mwakani Ujerumani inatarajia kufanya maonesho na Makumbusho ya Taifa ya Tanzania.

Naye Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii amempongeza Rais wa Ujerumani kwa kutembelea Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea ambapo amesema hilo ni tukio la kihistoria kwa Rais wa Ujerumani kutembelea makumbusho hiyo.

Amesema serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii ipo tayari kutumia historia ya vita ya Majimaji kwa faida ya kijamii na kiuchumi kwa nchi za Tanzania na Ujerumani

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo Mbunge wa Songea mjini ambaye pia ni Waziri waUtamaduni,Sanaa na Michezo,Dkt.Damas Ndumbaroamesema  nchi za Tanzania na Ujerumani zinapaswa kutengeneza mahusiano  na ushirikiano mzuri na kusahau yaliyopita kwenye vita ya Majimaji.

Ametoa rai kwa nchi zote mbili kushirikiana na kuleta maendeleo katika mji wa Songea na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla ambapo alisisitiza wananchi wa Songeakuona makumbusho ya kisasa kati ya Ujerumani na Songea yakijengwa mjini Songea.

Amesema ziara ya Rais wa Ujerumani mjini Songea nihatua muhimu sana ya kuleta maridhiano na mahusiano mazuri ya kijamii na kiuchumi baina ya nchi hizo .

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.