• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RAS RUVUMA atahadharisha utoaji takwimu zisizo sahihi

Imewekwa kuanzia tarehe: October 9th, 2024

Na Gustaph Swai- Rs Ruvuma

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bi. Mary Makondo ametahadharisha kuwa takwimu zisizo sahihi zinaweza kusababisha upotevu wa rasilimali  na kuchelewesha maendeleo yanayotakiwa kuonekana katika jamii

Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya Mfumo wa fursa na vikwazo kwa maendeleo (O&OD) Ulioboreshwa kwa Waratibu wa Mfumo huo kwa Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

"Takwimu zisizo sahihi zinaweza kusababisha upotevu wa rasilimali na kuchelewesha maendeleo tunayotamani kuyaona katika jamii", Alisema.

Amewataka Waratibu hao kutoa takwimu sahihi na kufanya kazi ili kuwa na taarifa zilizo sahihi kwani matarajio kuanzia ngazi ya Taifa hadi Msingi ni makubwa na wananchi wanahitaji maendeleo.

Amewaagiza wataratibu kuandaa taarifa mapema, kuzikamilisha na kuziwasilisha kwa wakati na kufanya kazi kwa weledi  kwani bila ya kuwa na taarifa ni sawa na kutokufanya kazi na kushindwa kuwajibika jambo ambalo ni kosa.

Ametoa rai kwa Waratibu hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani hali hiyo inachelewesha kufikiwa kwa malengo ya Serikali  na kuwakosesha Wananchi maendeleo na kuwataka kubadilika na kujipanga vyema kufanya kazi kwa ufanisi.

Sanjari na hayo ameeleza kuwa Mfumo wa fursa na vikwazo ulioboreshwa ni moja ya  juhudi zinazofanywa na Serikali kwa ajili ya kuwajengea uwezo Wananchi ili Kuwaongezea ari ya ushiriki kwa kupanga na kusimamia shughuli za maendeleo.

Amelitaja lengo la maboresho ya Mfumo huo kuwa ni kuhakikisha wanaweza kutatua changamoto zilizokuwa katika mfumo wa awali kama vile ushiriki hafifu, jamii kukosa Moyo wa umiliki wa miradi na kuongezeka kwa utegemezi wa jamii kwa Serikali.

Amesema mfumo huo ni nyenzo muhimu katika mchakato wa maendeleo ya jamii zetu hivyo unatarajiwa kuleta faida za Moja kwa Moja katika kuleta utoaji wa huduma na maendeleo  endelevu.

Naye Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Ruvuma Ndg.Jumanne Mwankhoo amewasisitiza Waratibu kubadilika na kujenga Utamaduni wa kufanya kazi bila kuhimizwa.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.