• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC azindua Baraza la Wazee Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: September 3rd, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amezindua Baraza la Wazee Mkoa wa Ruvuma katika hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Songea Klabu.

Akizungumza kabla ya uzinduzi huo,Kanali Thomas amesema serikali imekuwa ikitoa huduma kwa wazee kwa kuzingatia sera ya Taifa ya wazee ya m waka 2003 na Sera ya Afya ya mwaka 2007, sanjari na miongozo mbalimbali ili kuhakikisha wazee  wanastawi vyema bila kubaguliwa.

“Sote tunafahamu suala la uzee na kuzeeka limekuwa lenye umhimu mkubwa kwa Taifa hasa kuhusiana na mitazamo ya kiuchumi,kisiasa na kijamii’’,alisisitiza Kanali Thomas.

Hata hivyo amesema wazee ni moja ya kundi lilikuwa limetengwa katika jamii hivyo nguvu za ziada kutoka serikalini na wadau kwa ujumla zimeendelea kufanyika ili kuhakikisha wazee wanapata haki zao za msingi.

Mkuu wa Mkoa amesema tayari Mkoa umewatambua wazee  katika ngazi zote  ambapo jumla ya wazee 96,054 walitambuliwa katika Mkoa kwa lengo la kuhakikisha wanapatiwa huduma muhimu zikiwemo matibabu bure.

Amesema uundaji wa mabaraza ya wazee umefanyika katika Halmashauri zote nane ambapo takwimu zinaonesha kuwa yameundwa mabaraza katika kata 173,vijiji na mitaa 686 ,Halmashauri nane na Baraza la wazee la Mkoa ambalo linazinduliwa leo.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma Viktor Nyenza akitoa taarifa ya huduma ya wazee amesema jumla ya wazee 43,312 wamepatiwa vitambulisho vya matibabu bure saw ana asilimia 45 na wazee 5,384 wananufaika na huduma za bima ya afya.

Nyenza amesema Mkoa unasimamia utoaji na upatikanaji wa huduma bora za matibabu bila malipo kwa wazee wote kwenye vituo vya kutolea huduma za afya vinavyomilikiwa na serikali.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Ruvuma Ezieli Nyoni akizungumza kwa niaba wazee mara baada ya uzinduzi wa Baraza hilo,amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuzindua Baraza hilo ambalo liliundwa Juni 2021.

Amesema sasa Baraza limepata nguvu na lipo tayari kuanza kazi ya kuwatumika wazee hasa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee.

Amezitaja baadhi ya changamoto za wazee kuwa ni upungufu wa baadhi ya bidhaa za afya kwa ajili ya matibabu ya wazee,umasikini na hali duni kiuchumi kwa wazee na uwepo wa Imani potofu za kishirikina zinazotishia usalama wa wazee katika baadhi ya maeneo.

Kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012,idadi ya wazee Tanzania imeongezeka kufikia milioni 3.1 ukilinganisha na wazee milioni 1.4 mwaka 2002.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ruvuma

Septemba 3,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.