• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC IBUGE aagiza wodi tatu za hospitali ya Songea kukamilika kwa wakati

Imewekwa kuanzia tarehe: June 2nd, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Songea kuhakikisha ujenzi wa wodi tatu za hospitali ya  wilaya hiyo unakamilika ndani ya mkataba ili wananchi waanze kupata huduma mapema.

RC Ibuge ametoa agizo hilo baada ya kukagua mradi huo ambao serikali imetoa shilingi milioni 500 kutekeleza mradi huo ambao ujenzi wake umeanza Mei 23 mwaka huu na unatarajia kukamilika Novemba mwaka huu.

“Naagiza twende kwa spidi lakini kazi iwe yenye ubora,mimi ninapofanya ziara huwa sitoi taarifa,nitarudi wakati wowote,nikikuta jengo halina ubora,nitabomoa kwa gharama yako’’,alisisitiza Brigedia Jenerali Ibuge.

Kabla ya kukagua mradi huo,RC Ibuge alikagua majengo saba ya hospitali ya wilaya ya Songea ambayo yamejengwa katika kijiji cha Mpitimbi na kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.8 ambapo ameagiza majengo yote yaanze kutoa huduma  ikiwemo huduma ya upasuaji.

RC Ibuge amesema serikali imetumia gharama kubwa kujenga majengo ya hospitali hiyo,ambapo amesisitiza yasipotumika itakuwa sawa na kazi bure hivyo amewaomba madiwani wa Halmashauri hiyo,kushirikiana ili kuhakikisha hospitali hiyo  inaanza kutoa huduma za afya mapema.

Awali akitoa taarifa ya mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Dr.Gofrey Kihaule amesema serikali ilitoa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa hospitali hiyo ambapo mradi ulianza kwa majengo saba.

Ameyataja majengo hayo kuwa ni majengo ya wagonjwa wa nje (OPD),utawala,mionzi ,kufulia,bohari ya dawa na jengo la upasuaji ambalo linahusisha mama na mtoto na kwamba ujenzi uliendelea mwaka 2020 ambapo serikali ilitoa shilingi milioni 300 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi ikiwemo  ujenzi wa njia za kupitishia wagonjwa.

Hata hivyo Dr.Kihaule amesema ujenzi wa hopsitali hiyo ulikamilika Julai 2020 ambapo huduma za matibabu kwa wagonjwa wa nje zilianza kutolewa rasmi na kwamba katika bajeti ya mwaka 2020/2021 Halmashauri imepokea milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa wodi tatu ambazo ni wodi ya watoto,wanawake na wanaume.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Juni pili,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.