• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC IBUGE aipongeza Manispaa ya Songea kwa kupata hati safi

Imewekwa kuanzia tarehe: June 20th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Generali “Balozi” Wilbert Ibuge amewapongeza Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Songea kwa kukusanya mapato ya ndani kwa zaidi ya asilimia 99.01%.

Hayo yamebainishwa katika kikao cha baraza Maalum la Madiwani  kilichofanyika leo 18 Juni 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kupitia taarifa za Mkaguzi Mkuu wa ndani  wa hesabu za Serikali (CAG)  kwa mwaka wa fedha 2019/2020,  kikao kilichohudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani wa kata zote 21 zilizopo katika Manispaa ya Songea, wakuu wa Idara na viongozi mbalimbali.

Akitoa pongezi hizo Ibuge amesema,   Halimashauri ya Manispaa ya Songea katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 imekusanya  kiasi  cha Tshs. 3,374,756,150.90/= kati ya kiasi kilichotarajiwa kukusanywa ambacho ni Tshs. 3,408,416,455/=  nakufikia lengo kwa asilimia 99.01%.

Alibainisha kuwa,  Halmashauri ya Manispaa ya Songea  imechangia Tshs. 286,304,029/= ambayo ni sawa na asilimia 98.17%  kwa ajili ya kuwezesha  mfuko wa wanawake 4%, vijana 4%  na watu wenye ulemavu 2%,  fedha ambayo  imesaidia kutoa fursa  kwa vijana kujiajiri  wenyewe pamoja  na kuleta  maendeleo kwa jamii.

Alisema  “ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi Mkuu Mkazi  wa hesabu za Serikali  umetekelezwa vizuri  na kufanikisha kujibu hoja zilizotolewa kwa zaidi ya asilimia 95% kati ya hoja zilizotolewa na kupelekea Halmashauri  ya Manispaa Songea kupata hati safi. Pia   Amewataka viongozi  hao  kuhakikisha wanamaliza kujibu hoja zote ambazo  bado hazijakamilika kufungwa  hadi kufikia tarehe 30 Septemba ziwe zimejibiwa. “ Aliwapongeza.”

 Ametoa  Rai kwa Waheshimiwa Madiwani na wataalamu  kushiriki ipasavyo kujibu hoja zote pamoja na kutekeleza maelekezo wanayopewa kutoka kwa Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali wa ndani na kutoruhusu marudio ya hoja zilezile ambazo hujitokeza kila mwaka.  “Ibuge Alieleza”

Aidha amewataka Waheshimiwa Madiwani kuhakikisha wanatekeleza ahadi walizoahidi kwa wananchi katika kipindi cha kampeni  na kusimamia vizuri miradi mikubwa iliyokamilika  ikiwemo na stendi ya Tanga na machinjio  ya kisasa ambayo imeanza kutumika ambapo inasaidia kuongeza mapato na kuleta maendeleo katika Halmashauri  na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Ibuge ameziagiza Halmashauri zote  Mkoani Ruvuma kuhakikisha wanalipa madeni yote  ya wazabuni kwa wakati,  kuendesha  vikao vya ukaguzi vya mapato  ya ndani  mara kwa mara kwa mujibu wa sheria. Wakurugenzi wote kila Halmashauri husika  watahakikisha  wanashiriki vikao vya ukaguzi pamoja na Waheshimiwa Madiwani ili kuleta ushirikiano wa pamoja  na kutatua changamoto za Halmashauri husika.’Alisisitiza’

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano amesema kuwa Baraza la Madiwani limejipanga kusimamia miradi ya maendeleo pamoja na kuyafanyia kazi maelekezo yaliyotolewa na Serikali katika kuhakikisha wanaleta maendeleo katika Manispaa ya Songea.

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.