• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC Ibuge akusudia kuimarisha uhifadhi maliasili

Imewekwa kuanzia tarehe: February 8th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema amedhamiria kuimarisha usimamizi, ulinzi na uhifadhi Maliasili kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Ibuge amesema Mkoa umekuwa katika mstari wa mbele katika kuwahamasisha wananchi juu ya utunzaji wa mazingira kwa kutokuchoma misitu hovyo na upandaji wa miti katika maeneo yaliyo wazi na kwenye vyanzo vya maji.

Hata hivyo Ibuge amesema Mkoa wa Ruvuma unalengo la kupanda miti ya biashara eka 100,000 na kwamba Mradi huu unatekelezwa kwa kupanda miti maeneo ya serikali kuu, serikali za mitaa, mashuleni pamoja na vijijini.

RC Ibuge amesema Mkoa una mpango wa kuanzisha mashamba ya wanyamapori kwenye jumuiya tano, Kisiwa cha Lundo pamoja na chuo cha Maliasili cha  Likuyusekamaganga ili wananchi wajifunze toka hapo na kuanzisha mashamba binafsi.

Ameishukuru serikali kwa kuboresha miundombinu ya barabara na anga na hivyo kuufungua Mkoa na kuchochea shughuli za maendeleo ikiwemo utalii.

‘’Mkoa kwa kushirikiana na WWF tumeandaa mpango wa kukuza Utalii, kutengeneza filamu fupi ya matangazo, vipeperushi pamoja na jarida la kuonyesha vivutio vya Mkoa ’’,amesema Brigedia Jenerali Ibuge.

Hata hivyo Ibuge amesisitiza kuwa baada ya Mkoa kubaini kuna vyanzo vya maji vinaharibiwa na shughuli mbalimbali za wananchi,ameutaja mpango uliopo sasa ni kuhakikisha kuwa vyanzo vyote vya maji vinakabidhiwa kwa Wakala wa Misitu TFS ili viweze kupimwa, kuwekewa mipaka pamoja na kupanda miti kwenye vyanzo vya maji.

Imeandaliwa na Bahati Nyoni

Kutoka Ofisi ya Habari ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma   

Februari,8 2022.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.