• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC IBUGE atoa maagizo mazito kwa wasafirishaji kukabiliana na UVIKO 19

Imewekwa kuanzia tarehe: August 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ameviagiza vyombo vyote vya usafirishaji abiria yakiwemo malori,kuhakikisha wanaweka vipukusa mikono(sanitizers) ili kupunguza maambukizi ya UVIKO 19.

RC Ibuge ametoa maagizo hayo wakati anafunga kikao cha wadau wa usafiri na usafirishaji kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea  ambapo pia yamepitishwa maazimio ambayo yanahitaji utekelezaji wa pamoja.

Maazimio na maelekezo mengine ni  lazima abiria wote wavae barakoa ambapo  RC Ibuge amesisitiza ni lazima kila mmoja kulinda afya yake na ni wajibu wa kumlinda mwingine dhidi ya UVIKO 19.

“Ukikiuka kumlinda mwingine maana yake umevunja sheria na ni kosa la jinai ambalo halina tofauti na kukusudia kuua kwa hiyo sio hiari,unapopanda chombo cha moto uhakikishe una barakoa’’,alisisitiza Ibuge.

Mkuu wa Mkoa pia ameagiza kila stendi ya mabai ziwekwe ndoo za kutosha zenye maji tiririka na sabuni kwenye maeneo muhimu ya kuingilia na kutoka magari na yeyote ambaye anakiuka afikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Ameagiza elimu endelevu ya kukabiliana na UVIKO 19 itolewe na wataalam wa afya kupitia redio za kijamii zilizopo mkoani Ruvuma ili wananchi wapate uelewa wa kutosha kuhusu ugonjwa huo.

Hata hivyo amesema stendi ya Mfaranyaki mjini Songea isitumike kubeba abiria kwa sababu ya kuwepo kwa kituo cha mafuta ambacho kinaweza kusababisha maafa makubwa kwa wananchi likitokea tatizo kama moto

Akizungumzia utekelezaji wa sheria ya abiria kufunga mikanda na abiria wote kukaa kwenye viti bila kusimamishwa,Brigedia Jenerali Ibuge amesema ni muhimu kuzingatia sheria  ili kupunguza msongamano kwenye vyombo vya abiria hivyo kupunguza maambukizi.

Kuhusu madereva bodaboda kubeba abiria zaidi ya mmoja,Mkuu wa Mkoa amesema suala hilo halina mjadala ni marufuku kubeba mishikaki na kwamba kofia kwa abiria ni lazima ili kujikinga.

Ametoa rai kwa wananchi wote mkoani Ruvuma kuchanja chanjo ya UVIKO 19,hata hivyo amesema chanjo hiyo ni hiari na kwamba chanjo hiyo  imethibitika kitaalam inasaidia kushitua kinga ya mwili kukabiliana na UVIKO 19 hivyo kupunguza vifo au mgonjwa kuzidiwa hadi kuwekewa gasi ya kupumlia.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Agosti 6,2021

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.