• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC IBUGE;Wataalamu wa afya Ruvuma toeni elimu endelevu kwa wananchi kujikinga na corona

Imewekwa kuanzia tarehe: July 14th, 2021

RC IBUGE;WATAALAMU WA AFYA TOENI ELIMU ENDELEVU YA KUJIKINGA NA CORONA KWA WANANCHI

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ameziagiza Halmashauri zote nane kupitia wataalam wa afya kusimamia kutoa elimu ya kujikinga na  maambukizi ya wimbi la tatu la corona.

RC Ibuge ametoa maagizo hayo wakati anazungumza na  wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa Halmashauri na watumishi wa umma ngazi ya Mkoa na wilaya zote kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Amesisitiza elimu endelevu ya kujikinga kabla ya kuugua  corona itolewe kwa wananchi ikiwemo kuvaa barakoa,matumizi ya kunawa kwa sabuni na maji titirika na kuepuka mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.

“Nimepita na kuzunguka baadhi ya maeneo mjini Songea,nimeona wananchi wameacha zile hatua ambazo tulikuwa tumezichukua katika wimbi la kwanza mfano,nje ya maeneo ya huduma,ndoo hazina maji wala sabuni,tukasimamie kuwaelimisha wananchi kwa sababu kujikinga ni gharama ndogo kuliko kutibu’’,alisisitiza RC Ibuge.

Amesisitiza kuwa corona ipo nchini,ingawa amebainisha kuwa katika Mkoa wa Ruvuma tishio la corona sio kubwa,hata hivyo amesema hakuna mipaka iliyofungwa  hivyo kuna mwingiliano mkubwa wa watu kusafiri na kuingia ndani ya Mkoa wa Ruvuma hivyo elimu endelevu ya kujikinga na corona isimamiwe ipasavyo kwa wananchi.

“Suala la  kujikinga ni rahisi kuonekana halina umuhimu kama madhara bado hatujayaona,sote tumekuwa tukisikia maelekezo mbalimbali kutoka Wizara ya Afya na kupitia viongozi wa kitaifa akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,wimbi la tatu la corona tayari lipo nchini tuchukue tahadhari’’,alisema RC Ibuge.

Takwimu kutoka Wizara ya Afya zinaonesha kuwa hadi sasa Tanzania ina wagonjwa wa corona 408 waliothibitika kutoka baadhi ya mikoa hapa nchini.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 14,2021 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.