• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC MNDEME akagua miradi ya maji yenye thamani ya sh.bilioni mbili na milioni 670 inayotekelezwa Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: July 6th, 2020

Wilaya ya Namtumbo inavyotekeleza miradi miwili ya maji yenye thamani ya  zaidi ya sh.bilioni mbili na milioni 670 

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amekagua miradi miwili ya maji ya Mkongogulioni na Milonji kata ya Lusewa  wilayani Namtumbo  inayotekelezwa na serikali kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni mbili na milioni 670.

Akitoa taarifa ya mradi wa maji wa Milonji  Kata ya Lusewa,Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo David Mkondya amesema mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 612.

Hata hivyo amesema mradi huo  chanzo chake ni kisima kirefu na maji yake yanasukumwa kwa nguvu za jenereta na kwamba mradi unatekelezwa na Mkandarasi BERAS INVESTMENT LTD kuanzia mwaka 2013 hadi 2015 ambao unatarajia kuhudumia watu 4988 katika kijiji cha Milonji.

Hata hivyo Mkondya amesema mradi huo unakabiliwa na changamoto za mwamko mdogo wa wananchi katika uchangiaji wa mfuko wa maji na kwamba RUWASA wilaya ya Namtumbo   inaendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa kuchangia mfuko wa maji na kufanya ufuatiliaji  na usimamizi  kwa jumuiya ya watumiaji maji.

“Tangu mradi umekamilika  mwaka 2015, kwa miaka mitano wananchi walikuwa wanakataa kuchangia mfuko wa maji kwa ajili ya mafuta ya jenereta  hali iliyababisha kuendelea kutumia maji ya mtoni na visima ambayo sio safi na salama ‘’,alisema Mkondya.

Akizungumzia mradi wa maji ya Mkongogulioni na Nahimba,Kaimu Meneja wa RUWASA amesema mkataba wa mradi huo unagharimu zaidi ya shilingi bilioni mbili  na ulitarajiwa kukamilika  Februari mwaka huu chini ya Mkandarasi Kipera Contructors LTD.

Amezitaja kazi ambazo zimepangwa kufanyika kulingana na mkataba kuwa ni  ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 25,000 katika kijiji cha Nahimba,ukarabati wa matanki mawili  moja likiwa na ujazo wa lita 150,000 katika kijiji cha Mkongo na lingine lita 25,000 katika kijiji cha Nahimba.

Kazi nyingine zinazofanyika kwenye mradi huo ni uchimbaji wa mitaro ya maji laini kuu  urefu wa kilometa 15 na laini ya usambazaji kilometa 17.84,ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 46 ambapo baadhi ya maeneo yameanza kupata huduma ya maji ikiwemo kitongoji cha Litete kata ya Mkongogulioni.

Amezitaja kazi ambazo zinaendelea katika mradi huo kuwa ni ulazaji  wa mtandao mpya wa usambazaji maji katika kijiji cha Mkongogulioni ambapo mradi huo hivi sasa unakamilishwa na RUWASA kwa njia ya force akaunti,baada ya Mkandarasi kuchelewa kukamilisha na kwamba utekelezaji wake umefikia asilimia 85 na huduma ya maji imeanza kutolewa baadhi ya maeneo.

Akizunguma mara baada ya kukagua miradi hiyo ya maji,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema amesikitishwa na wananchi wa kijiji cha Milonji kushindwa kutumia maji tangu mradi ulipokamilika mwaka 2015 badala yake wananchi wameanza kutumia maji mwaka 2020.

“Watu 5000  katika kijiji cha Milonji wamekuwa hawapati maji kwa miaka mitano kwa sababu ya kuvutana,elimu ya  umuhimu wa kuchangia maji imetolewa kwa miaka mitano,somo halikueleweka, anayepata shida ni mama na watoto ambao wanasafiri umbali mrefu kuchota maji’’,alisema Mndeme.

Amesema serikali ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Ruvuma imetoa shilingi bilioni 30 za kuboresha sekta ya maji katika na kwamba kati ya fedha hizo,wilaya ya Namtumbo pekee imepokea zaidi ya bilioni 13 kwa ajili ya utekelezaji wa  miradi ya maji.

Ili kukabiliana na changamoto ya jenerata la kusukuma maji katika mradi huo,Mndeme amesema serikali mwaka huu inatarajia kufikisha umeme wa REA katika vijiji vyote ambavyo havijapata huduma hiyo,kikiwemo kijiji cha Milonji.

Mkuu wa Mkoa amewaasa wananchi hao kuendelea kuchangia kiasi cha shilingi 50 kila kaya kwa ndoo kwa ajili ya kununua mafuta ya kusukuma maji na kupata lita laki moja kwenye tanki kwa ajili ya matumizi ya wananchi  katika kipindi hiki cha mpito wakati wanasubiri umeme wa TANESCO.

Akizungumza na wananchi wa mradi wa maji ya Mkongogulioni, Mndeme amesema  serikali iliamua kumnyan’anya Mkandarasi kazi mradi huo kutokana na kuuchelewesha na kuamua ujengwe kwa nguvu za wananchi  kwa kutumia force akaunti.

Vijiji vya Kata ya Mkongogulioni na Milonji kata ya Lusewa wilayani Namtumbo havijawahi kupata maji safi na salama ya bomba tangu nchi kupata uhuru mwaka 1961.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 6,Namtumbo

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.