• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC MNDEME atoa rai kwa waumini kuendelea kuliombea Taifa,achangia 900,000 ujenzi wa nyumba ya padre

Imewekwa kuanzia tarehe: October 19th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ametoa rai kwa waumini kuendelea kuliombea Taifa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu ili uweze kufanyika kwa amani na utulivu.

 Mndeme ametoa rai  Jumapili hii aliposhiriki Ibada  na waumini wa Kanisa Anglikana Mtakatifu  Nicholaus lililopo mjini Songea.

Mkuu wa Mkoa ambaye pia amechangia Ujenzi wa Nyumba ya Mchungaji  saruji tani tatu yenye thamani ya zaidi ya shilingi 900,000,amewashukuru waumini wote kwa kuliombea Taifa la Tanzania kuanzia kipindi cha corona na hata kipindi hiki cha  kuelekea Uchaguzi Mkuu ambao unatarajia kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.

“Ndugu zangu nianze kuwashukuru kwa maombi yenu mnayoliombea Taifa hili,mkimuombea Rais wetu, mkiwaombea Mawaziri na viongozi wote wenye mamlaka katika nchi hii tunawashukuru sana maombi yenu yameifanya nchi yetu kuendelea kuwa na amani’’,alisema.

Hata hivyo Mndeme amesema  umebaki muda mchache kuelekea Uchaguzi Mkuu hivyo amewaomba waumini kuendelea kuliombea Taifa la Tanzania ili Mwenyezi Mungu ausimamie uchaguzi ufanyike kwa amani na nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani.

“Ndugu zangu tarehe 28 mwezi huu, Taifa letu la Tanzania linataingia katika uchaguzi  mkuu wa Rais ,wabunge na Madiwani, Niwaombe,naomba tujitokeze kwa wingi ili tukachagua viongozi wapenda maendeleo watakaoliongoza Taifa hili katika kipindi kingine cha miaka mitano’’,alisema Mndeme.

Mndeme amewasisitiza Watanzania ifikapo Oktoba 28 kila mmoja achukue maamuzi sahihi kuchagua viongozi sahihi  na wanaopenda maendeleo  na nchi ya Tanzania iendelee kuimarika katika Nyanja zote.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Ushirika wa Mama wa Kristo (UMAKI) katika Kanisa la Anglikana Agnes Hinjo, amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuja kuabudu katika ibada hiyo na kumuahidi kwamba wataendelea na maombi ya kuliombea Taifa la Tanzania siku zote.

“Sisi waumini wa Kanisa la Anglikana tupo kwenye maombi,UMAKI tumeamua kuchukua hatua za kuendelea na maombi   tangu aliposema Rais Magufuli tufunge kwa ajili ya corona,hatujaacha,tupo kwenye maombi kwa ajili ya uchaguzi’’,alisema Hinjo.

Naye Mchungaji wa Kiongozi wa Kanisa hilo Padre Mathayo Chanangula katika mahubilri yake kwenye ibada hiyo amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kazi njema anayofanya ya kusimamia masuala ya kimwili na kiroho.

Padre Chanangula amesema msaada wa saruji ambao  ameutoa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mchungaji utasaidia sana katika ukamilishaji wa nyumba hiyo ambayo itamwezesha Mchungaji kufanya kazi za kiroho kwa ufanisi zaidi.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka ofisi ya Habari ya Mkoa wa Ruvuma 

Oktoba 18,2020.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MSIKIMBILIE hasara,serikali inakuja na bei ya neema kwa mahindi Julai

    May 31, 2025
  • WAKULIMA Namtumbo wachuma neema ya ufuta kwa teknlojia mpya ya mnada wa kidigitali

    May 31, 2025
  • RUSHWA yazidi kuporomoka na kukosa nafasi Ruvuma

    May 31, 2025
  • SERIKALI yatoa fidia ya bilioni 2.5 kupisha mradi wa umeme wa Grid Songea-Tunduru

    May 31, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.