• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC MNDEME azipongeza Halmashauri sita zilizopata hati safi mkoani Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: June 20th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amezipongeza halmashauri sita kati ya nane zilizopata hati safi mkoani Ruvuma.

Mndeme ametoa pongezi hizo wakati anazungumza katika kikao kazi cha  majumuisho cha kujadili taarifa ya CAG kuhusu hoja na mapendekezo ya Hesabu za serikali kwa mwaka 2018/2019 kilichofanyika Ikulu ndogo mjini Songea.

Kikao hicho kilijumuisha wakurugenzi wa Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma,wakuu wa wilaya zote tano,makatibu tawala wote na watalam ngazi ya Halmashauri na Mkoa.

Mndeme amezitaja Halmashauri ambazo zimepata hati safi kwa miaka mitatu na miaka minne mfululizo kuwa ni Halmashauri ya Wilaya ya  Tunduru,Halmashauri ya Namtumbo,Madaba,Nyasa,Halmashauri ya Mji Mbinga na Halmashauri ya Wilaya ya Songea,

“Kwa Halmashauri mbili  za Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Songea zilizopata hati zenye mashaka,tunazielekeza zijipange upya na kuhakikisha ukaguzi wa 2019/2020 zinapata hati safi’’,alisisitiza.

Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuwa hati zenye mashaka na hati chafu hazikubaliki katika Mkoa wa Ruvuma ambapo ameagiza wote waliosababisha kupatikana kwa hati hizo wanatakiwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anawajibika katika matumizi sahihi ya fedha za umma na kuzuia hoja.

Katika ukaguzi wa CAG katika kipindi hicho kwa Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma kulikuwa na hoja na mapendekezo 496 ya miaka ya nyuma ambayo yalikuwa hayajafungwa.

Hata hivyo Mndeme amesema hadi kufikia Machi mwaka huu baada ya zoezi la uhakiki kufanyika kiasi cha hoja na mapendekezo 240 yamefungwa na kubakiza 256 ambayo bado yanaendelea kufanyiwa kazi kwa kupeleka vielelezo kwa ajili ya uhakiki.

Katika kikao hicho cha majumuishi wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma walitoa taarifa kuhusu hatua ambazo wamezichukua kwa watumishi waliosababisha hoja  zikiwemo watumishi hao kuwapa onyo la mdomo na onyo la maandishi.

Imeandikwa na  Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 19,2020

Ikulu Ndogo Songea

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.