• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC Mndeme:Serikali inatambua na kuthamini mchango wanawake katika jamii

Imewekwa kuanzia tarehe: March 9th, 2021

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na wanawake katika ujenzi wa Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme katika maadhimisho ya kilele ya siku ya wanawake Duniani  Mkoani Ruvuma yaliyofanyika katika kijiji cha Kalanje wilayani Tunduru.

Mndeme amesema kutokana na serikali kutambua umuhimu wa wanawake imeziagiza Halmashauri zote kutenga asilimia nne ya mapato yake ya ndani kwa lengo kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Amesema katika kipindi cha kuanzia Julai 2020 hadi Februari 2021 katika Mkoa wa Ruvuma,serikali imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi 444,167,441.82 kwa vikundi 603 vya wanawake,vikundi 221 vya vijana na vikundi 203 vya watu wenye ulemavu.

“Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatekeleza kauli mbiu hii ya Wanawake katika uongozi chachu kufikia dunia yenye usawa hivyo kwa vitendo, tunaona wakuu wa Mikoa/Mawaziri,wakuu wa Wilaya,Wakurugenzi na wakuu wa Idara ambao ni wanawake ni jukumu letu kuwapa wanawake nafasi ya uongozi”,alisisitiza Mndeme.

 Mndeme ameitaja siku ya wanawake kuwa ni muhimu sana kwa sababu  inaonesha nafasi kubwa waliyonayo wanawake katika jamii yetu na katika uongozi na kutoa mchango mkubwa wa malezi ya watoto.

Amesema wanawake ni nguzo kubwa katika nchi kwa sababu wanatoa dira na mwelekeo wa maendeleo katika ngazi zote za kifamilia hadi uongozi wa juu ya nchi.

Awali Afisa maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Ruvuma Zawadi Nyoni akitoa historia fupi ya siku ya wanawake duniani amesema ilianzishwa mwaka 1900 kufuatia maandamano ya wanawake wafanyakazi wa sekta ya viwanda nchini Marekani kupinga mazingira duni ya kazi.

Nyoni amesema wanawake walipinga ukosefu wa huduma za kijamii na kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji katika ajira ikiwemo wanawake kulipwa mshahara mdogo kwa kazi sawa ukilinganisha na wanaume.

Hata hivyo amewapongeza wanawake wa Mkoa wa Ruvuma kwa kuwa mstari wa mbele katika Nyanja za kuleta maendeleo endelevu kwa Jamii ikiwemo kushiriki na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Amesema wanawake wamekuwa mstari wa mbele kulaani vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake na watoto hususani wa kike,kupinga matumizi ya dawa za kulevya,na kupambana na janga la UKIMWI na magonjwa ya mlipuko kwa kutumia elimu kwa jamii kwa njia ya sanaa.

kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani mwaka huu ni  Wanawake katika uongozi chachu ya kufikia dunia yenye usawa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Madaba

Machi,9,2021

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.