• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA aagiza Halmashauri ya Nyasa kubuni vyanzo vipya vya mapato

Imewekwa kuanzia tarehe: September 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewaagiza watendaji katika Halmashauri ya Nyasa kuhakikisha wanabuni vyanzo vipya vya mapato ili kuongeza ukusanyaji mapato.

Kanali Thomas ametoa agizo hilo wakati anazungumza na watumishi,madiwani na wazee wa Wilaya ya Nyasa kwenye ukumbi wa chuo cha VETA mjini Mbambabay.

Mkuu wa Mkoa ameitaja wilaya Nyasa kuwa ni moja kati ya Wilaya tajiri mkoani Ruvuma ikiwa na maeneo ya madini ya aina mbalimbali yakiwemo madini ya makaa ya mawe ambayo yanaweza kuingizia wilaya hiyo mapato makubwa kupitia kodi iwapo usimamizi utakuwa wenye tija.

Amesema wilaya ya Nyasa kuanzia mwanzo wa wilaya hadi mwisho ina miamba ambayo ikiwekezwa inaweza kuongeza mapato makubwa katika Halmashauri hiyo.

“Wilaya ya Nyasa ndani ya ziwa Nyasa kuna Samaki wa aina mbalimbali zikiwemo aina 400 za Samaki wa mapambo,wanaovua Samaki hao wananufaika kwa sababu wanauzwa nje kwa Dola,hakikisheni Halmashauri inasimamia mauzo ya Samaki hao ili kuongeza mapato’’,alisisitiza Kanali Thomas.

Katika kuhakikisha mapato yanaongezeka kupitia sekta ya utalii Mkuu wa Mkoa amesema ziwa hilo limebarikiwa kuwa na fukwe zinazofaa kuwekeza ambazo zinavutia kuanzia Chiwindi mpakani na    nchi ya Msumbiji hadi Lituhi mpakani na  wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.

Kanali Laban pia ameagiza zoezi la usajiri wa wakulima liendelee ambapo hadi sasa ni wakulima 5000 tu wamesajiriwa katika wilaya ya Nyasa kati ya 16,000.

 Ameagiza kilimo cha Pamoja kipewe kipaumbele ambacho kinawawezesha wakulima wengi kulima zao la aina moja katika sehemu moja.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewaagiza ,madiwani katika Halmashauri hiyo kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo ukiwemo mradi wa maji wenye thamani ya shilingi bilioni 4.7 unatekelezwa katika vijiji vya Lituhi na Liuli.

RC Thomas amewaasa watumishi wa umma kuhakikisha wanajenga mahusiano mazuri ili utendaji wao uwe na tija pia amewataka kuacha kujiingiza kwenye madeni mengi yasiyokuwa na tija hali ambayo inashusha ari ya kufanyakazi.

Kuhusu changamoto zinazowakabili wazee zikiwemo za matibabu,ameagiza matibabu ya wazee yatolewe kwa wakati Pamoja na kuendelea kutoa vitambulisho vya matibabu bure kwa wazee,ingawa alitahadharisha kuwa Bima za afya zinazotolewa hazitoshelezi matibabu ya magonjwa yote.

Awali akizungumza kwenye kikao hicho,Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mheshimiwa Aziza Mangasongo alisema hadi sasa wazee waliotambuliwa kwenye wilaya hiyo ni 7528 kati yao waliopewa kadi za afya ni 4020.

Naye Mwenyekiti wa Wazee wa Wilaya ya Nyasa Yustine Mande akizungumza kwenye kikao hicho,amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kusikiliza kero za wazee na kuahidi kuzishughulikia.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma anaendelea na ziara ya kujitambulisha katika Halmashauri zote nane kwa kuzungumza na wazee,watumishi na  waheshimiwa madiwani.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ruvuma

Septemba 22,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.