• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA akagua miradi majengo mapya hospitali ya Rufaa ya Mkoa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 29th, 2024

 MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amekagua miradi ya ujenzi wa majengo ya hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma katika Kata ya Mwengemshindo Manispaa ya Songea.

Akitoa taarifa ya mradi huo,Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa,Songea Dr.Magafu Majura ameyataja majengo yanayotekelezwa kwenye mradi huo kuwa ni jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la huduma za mionzi na jengo la huduma za kuchuja damu(Dialysis unit).

Amesema kuwa serikali imetenga shilingi bilioni nne kujenga jengo la OPD  lenye ghorofa moja ambapo hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 75 na kwamba mradi unatarajia kukamilika katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.

Akizungumzia mradi wa jengo la mionzi,Dr. Majura amelitaja jengo la kutolea huduma za kichunguzi ya mionzi ambalo ndani yake kuna mashine mbili za CT Scan na Digital X ray ambazo zinazofanya kazi,limekamilika kwa asilimia 100 na limeanza kutoa huduma za CT Scan.

Dr.Majura ameutaja mradi wa huduma za kiuchunguzi za Radiolojia kuwa una thamani ya Zaidi ya shilingi bilioni mbili ambapo utekelezaji wa mradi huo ulianza Machi 2023 na huduma za CT Scan zilianza kutolewa Aprili 2023.

“Huduma ya CT Scan imepunguza adha kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma ambao walikuwa wanapata huduma hii katika hospitali ya Kanda ya Mbeya na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili’’,alisema Dr.Majura.

Mradi mwingine ambao unatekelezwa ni ujenzi wa jengo la  kisasa la kusafishia damu ambapo Dr.Majura amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Januari 2024 na unatarajia kukamilika Julai 2024 na kwamba jengo linagharimu shilingi milioni 600.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  amepongeza serikali kutekeleza miradi hiyo inayokwenda sanjari  na ununuzi vifaa vya kisasa katika hospitali hiyo  ambapo ametoa rai kwa wananchi kutumia huduma za kisasa zinazotolewa katika hospitali hiyo.

Amesisitiza kuwa wananchi wanachohitaji ni upatikanaji wa huduma na sio muonekano wa majengo ambapo amewataka watumishi kutunza majengo na vifaa.

 “Dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya afya karibu na tayari amefanya kwa kiwango kikubwa,utekelezaji wa Ilani umefanyika ,watendaji tuhakikishe majengo yote yanakamilika kwa asilimia 100’’,alisisitiza.

Ametoa rai kwa watumishi wote wa afya kutoa huduma kwa lugha rafiki kwa wagonjwa ambapo amesema kauli nzuri kwa wagonjwa zinampa matumaini ya kupona kabla ya kupata huduma.

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa hospitali 28 za Rufaa za mikoa ambapo historia yake inaanzia mwaka 1920,mwaka 1961 ilikuwa hospitali ya Wilaya,mwaka1964 ilipandishwa hadhi na kuwa hospitali ya Mkoa,Songea na mwaka 2009  ilitangazwa kuwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.