• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA akagua mradi wa maji wa bilioni 1.9 ,aagiza wananchi kuunganishiwa maji ndani

Imewekwa kuanzia tarehe: November 14th, 2023

Na Albano Midelo,Songea

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amekagua mradi wa maji katika Kijiji cha Lipaya Kata ya Mpitimbi wilayani Songea wenye thamani ya shilingi bilioni 1.9 na kuwaagiza RUWASA kuanza kuwaingizia ndani maji wananchi vijijini.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mkuu wa Mkoa,Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Songea Mhandisi Mathias Charles amesema mradi huo umesanifiwa ili kuwahudumia wananchi 3,886 kutoka katika vijiji vitatu na kwamba chanzo cha mradi huo kina uwezo wa kuzalisha maji lita 3,196,800 kwa siku.

“Mkataba wa mradi huu ni miezi 12 kuanzia Mei 2022 hadi Mei 2023,kutokana na changamoto zilizojitokeza mradi  haukukamilika hivyo umeongezewa hadi Januari 18,2024’’,alisema

Hata hivyo Mhandisi Charles amesema hadi sasa mradi umekamilika kwa asilimia 98 ambapo amezitaja kazi ambazo zimeshakamilika kwa asilimia 100 kuwa ni ujenzi wa vituo 17 vya kuchotea maji,ujenzi wa banio la maji,uzio, na ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa lita 100,000 ambalo limekamilika kwa asilimia 97.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewapongeza RUWASA kwa kuendelea kusimamia vema miradi ya maji hivyo kuunga mkono azma ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kumtua mama maji kichwani.

Amesisitiza kuwa nia ya Rais Dkt. Samia ni kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama ambapo amewaasa wananchi kuwa tayari kulipa bili za maji ili miradi ya maji iwe endelevu.

“Ili wananchi waweze kulipa bili zao kikamlifu,nakuaagiza Meneja wa RUWASA hakikisha wananchi wanaingiziwa maji ndani ya nyumba zao hivyo kinachotakiwa ni kutoa elimu kwa wananchi’’,alisema.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amekemea tabia ya uharibifu kwenye vyanzo vya maji ambapo amewaagiza  viongozi ngazi ya vijiji kuhakikisha wanashirikiana na Wakala wa Misitu Tanzania TFS kulinda vyanzo vya maji na kuzuia shughuli zote za kibinadamu kwenye chanzo cha maji cha Matogoro B wilayani Songea kinachotegemewa na Manispaa ya Songea.

Naye Diwani wa Kata ya Mpitimbi Mheshimiwa Issa Kindamba  amempongeza Rais Dkt.Samia kwa kutoa fedha nyingi za kutekeleza mradi huo ambao amesema unakwenda kupunguza umbali wa wananchi kutembea kufuata maji na kupunguza magonjwa yanayosambazwa na maji yasiyo salama.

Kukamilika kwa mradi huu kumeongeza upatikanaji wa maji safi na salama katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea kutoka asilimia 71.4 hadi kufikia asilimia 73.8

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.