• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA asikiliza kero za wananchi Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: April 14th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, ametembelea vituo vya mabasi vya Ruhuwiko na Mfaranyaki katika Manispaa ya Songea, kusikiliza kero, maoni, na mapendekezo ya wananchi pamoja na wafanyabiashara wa maeneo hayo.

Akiwa katika kituo cha mabasi cha Ruhuwiko, Kanali Ahmed amesisitiza umuhimu wa ushirikishwaji wa wadau wote, hususan wananchi na wafanyabiashara, katika mipango ya ujenzi wa stendi na vibanda vya biashara ambapo ametoa maagizo kwa wilaya na wataalamu kuhakikisha kuwa maamuzi yanayofanywa yanazingatia ushirikiano wa pande zote.

"Ninaagiza ushirikishwaji mkubwa wa wadau wote mliopo hapa, kama kuna suala la kutaka kuhamisha au kukodishwa vibanda, kuboresha huduma za bodaboda na bajaji, ni lazima ushirikishwaji mkubwa uwepo baina ya Serikali, chama na wenye hizo bodaboda, ili mtakayoyaamua yaweze kutekelezeka kirahisi kwa sababu yatakuwa ni maamuzi yaliyotokana na sisi sote," alisema Kanali Ahmed.

Pia amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika maamuzi na kutekeleza kwa haraka makubaliano yanayofikiwa, ili kuboresha eneo husika kwa manufaa ya jamii yote.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Kapenjama Ndile, ameeleza kuwa kituo cha mabasi cha Ruhuwiko kina umuhimu mkubwa kutokana na shughuli nyingi za biashara zinazofanyika hapo, hivyo amesema kuwa Manispaa ya Songea ina mipango madhubuti ya kuboresha eneo hilo.

Katika hatua nyingine, Meneja wa TANROAD Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Saleh Juma, amezungumzia msongamano wa magari unaosababishwa na malori mengi yanayobeba makaa ya mawe, akieleza kuwa ujenzi wa barabara mpya ya mchepuko (Songea Bypass) utaanza hivi karibuni.

Amebainisha kuwa tayari wananchi waliopo pembezoni mwa barabara hiyo wameanza kulipwa fidia ili kupisha ujenzi, hivyo amewahakikishia wananchi kuwa changamoto hiyo inashughulikiwa.

Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea, Mhe. Michael Mbano, amekiri changamoto ya vumbi na tope katika kituo cha mabasi cha Ruhuwiko wakati wa mvua, na amesisitiza kuwa hatua madhubuti zinaendelea kuchukuliwa ili kuimarisha mazingira ya eneo hilo.

Ameongeza kuwa Ruhuwiko ni eneo linalokua kwa kasi, na ni lango muhimu kwa wageni wanaoingia na kutoka mkoani kutokana na uwepo wa uwanja wa ndege.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.